BAADHI ya wanachama wa NCCR-Mageuzi wamemtaka Mwenyekiti wa chama hicho,
James Mbatia na Katibu Mkuu wa chama hicho, Martin Danda kujiuzulu
ndani ya siku tatu kutokana na tuhuma mbalimbali zikiwamo ubadhirifu wa
fedha na kutaka kukiua chama hicho.
Mbatia anadaiwa kuuza mali za chama zikiwamo nyumba mbili zilizoko
jijini Dar es Salaam eneo la Bunju B, moja iliyoko Tarime mkoani Mara na
shamba la ekari 56 lililoko Bagamoyo mkoani Pwani.
Faustine Sungura mmoja wa wanachama wa chama hicho, amesema mbali na
kuuza nyumba pia Mbatia ana mkakati maalumu wa kuiua NCCR na kuhamia
Chadema ambako ameahidiwa ukatibu Mkuu.
“Hivi sasa kuna mkakati wa kuuza nyumba nyingine za chama zilizopo
mkoani Rukwa na Katavi na mauzo yatakabidhiwa kwake kwa madai kuwa
anakidai chama fedha alizokikopesha wakati wa uchaguzi mkuu mwaka 2015,
tunatoa tahadhari kwa watu kutonunua nyumba hizo kwani watapata hasara
isiyotibika,” alisema.



0 comments :
Post a Comment