TAARIFA KUTOKA JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA


 kida
Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya limeendelea kufanya misako, operesheni na doria zenye tija katika maeneo mbalimbali ili kudhibiti uhalifu na wahalifu na limekuwa likishirikiana na wananchi na wadau wengine katika jitihada hizo za kukabiliana na uhalifu na wahalifu na kupata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kupungua kwa matukio makubwa ya uhalifu.
Aidha Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya limeendelea kukabiliana na matukio makubwa ya uhalifu pamoja na wahalifu. Jitihada zinaendelea kwa kushirikiana na wananchi kuhakikisha mkoa wetu unakua mahala salama. Hata hivyo kumekuwa na tukio moja la ajali ya kifo na majeruhi kama ifuatavyo :-
  • AJALI YA KIFO NA MAJERUHI.
Tarehe 06.02.2017 saa 20:45hrs eneo Inyala – Mablock, kata ya Inyala, tarafa ya Tembela, wilaya ya kipolisi Mbalizi, mkoa wa Mbeya. Gari T.688 DHE aina ya Yutong basi mali ya kampuni ya Super Feo ikitokea Mbeya mjini kuelekea Mbinga mkoa wa Ruvuma, ikiendeshwa na dereva aliyefahamika kwa jina la ABDALLAH MWINYIHERI, iliacha njia na kupinduka kisha kusababisha kifo cha abiria mmoja ambaye bado kutambuliwa, jinsi ya kiume, miaka kati ya 32 hadi 35 na majeruhi kwa ANNA MUHEZA [39], mkazi wa Mbeya na ANNA BRUNO [20], mwanafunzi chuo kikuu cha Mzumbe – Mbeya ambao wamelazwa hospitali ya rufaa Mbeya.  Chanzo cha ajali ni mwendo kasi, dereva alikimbia baada ya ajali.  Jitihada za kumtafuta zinaendelea.
Aidha kuna mafanikio yaliyopatikana katika misako ni kama ifuatavyo:-
  • KUPATIKANA NA UNGA UDHANIWAO KUWA NI DAWA ZA KULEVYA.
Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya linamshikilia  ANITHA ABEL [21],  mwanafunzi  kidato cha tatu wa shule ya sekondari Sanani iliyopo [W] Mbozi [M] Songwe akiwa na kete 15 za unga udhaniwao kuwa ni dawa za kulevya.
Tukio hilo limetokea  tarehe  30.01.2017 majira ya saa 12:00hrs katika  mtaa wa Mshikamano, kata ya Nsalala, tarafa ya Usongwe, wilaya ya kipolisi Mbalizi, mkoa wa Mbeya. Mtuhumiwa alikutwa katika harakati za kuuzia wateja dawa hizo na alipoona Polisi alikimbilia chooni ambapo hata hivyo alikamatwa. Taratibu za kisheria zinafanywa ili mtuhumiwa afikishwe mahakamani.
  • KUPATIKANA NA MALI YA WIZI.
Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya linawashikilia wafanyabiashara nane wakazi wa jijini Mbeya kwa kupatikana na mali ya wizi, vitenge jumla ya doti 1,075 kufuatia tukio la wizi lililofanyika jijini Dar es salaam.
           Tukio hili limetokea tarehe 06.02.2017 kati ya saa 11:00hrs hadi saa     15:00hrs eneo        la Mwanjelwa sokoni, kata ya Manga, tarafa ya Iyunga          jijini Mbeya. Watuhumiwa           waliokamatwa na idadi ya doti za vitenge       kwenye mabano ni DENIS CHAULA [           doti 168], SALOME MGAYA   [doti 102], MAHOMI SANGA MWAKYOSA        [doti 104], SUPE KANYAMALE [doti 66], JANE MAHELA [doti 62],       MATRIDA                      NGAILO [doti 171], TUKAE MAJIO [doti 163] na JULIANA   MAHENGE           [doti 239].
  • KUINGIA NCHINI BILA KIBALI NA KUSAFIRISHA WAHAMIAJI HARAMU.
Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya linawashikilia raia 7 wa Ethiopia kwa kosa la kuingia nchini bila kibali na pia wamekamatwa wasafirishaji watanzania wanne.
Tukio hili limetokea tarehe 31.01.2017 saa 02:40hrs kijiji cha Mpakani, kata ya Igawa, tarafa ya Rujewa, wilaya ya Mbarali, mkoa wa Mbeya. Watuhumiwa hao ni  [1]. SUJUMI  PARACHO [40],  [2]   ELIAS  HAVALA  [22].  [3] GETSO  TAVALA [25], [4]. TAMASKE  LARE,  [22], [5]. ZULFU MANGU [27], [6]. DABAVA  LAFIVU  [30],  na [7] SHETO  HERISO [25],  wote raia wa Ethiopia.
Katika tukio hilo wasafirishaji wa  wawahamiaji haramu hao ambao ni watanzania wanne walikamatwa wakitumia gari T.347 DAJ aina ya Toyota Caravan haice. Watuhumiwa hao  ni dereva 1. FILEX  MLAGILA  [32], 2.  ELIAS S/O ARON [30],  3. FRED S/O PETER,  [23] na  AZALIA S/O ELIAS,  [30] wote wakazi  wa Uyole
WITO:
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Naibu Kamishina wa Polisi DHAHIRI A. KIDAVASHARI  anatoa wito kwa jamii kuacha tabia ya kutumia dawa za kulevya kwani ni  kinyume cha sheria  na ni hatari kwa afya ya mtumiaji. Aidha Kamanda Kidavashari anaendelea kutoa wito kwa jamii kutoa taarifa juu ya mtu/ watu / kikundi au mtandao wa wanaojihusisha na utumiaji, usafirishaji na uuzaji wa dawa za kulevya ili hatua dhidi yao zichukuliwe mara moja.
Kadhalika Kamanda Kidavashari anaendelea kutoa wito kwa jamii hususan watumiaji wa barabara na madereva kuzingatia na kutii sheria za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuepukika.    Pia ametoa wito kwa yeyote mwenye taarifa juu ya mahali alipo dereva aliyesasababisha ajali na kukimbia azitoe katika mamlaka husika ili akamatwe, vinginevyo ajisalimishe mara moja.
Imesainiwa na :
[DHAHIRI A. KIDAVASHARI – DCP]
 KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment