• Home
  • PARADISE BLOG
  • Contact US
  • MAONI

Tz News Blog

Habari,Matukio,Picha ulimwenguni kote.



  • Home
  • KITAIFA
    • KIMATAIFA
    • Fashion2
  • KIMATAIFA
    • Sub Menu 1
    • Sub Menu 2
    • Sub Menu 3
  • JAMII
  • MICHEZO
  • SIASA
  • MAGAZETI
Home / KIMATAIFA / Israel Yapiga Marufuku Sauti Za Adhani Misikitini

Israel Yapiga Marufuku Sauti Za Adhani Misikitini

03:46 KIMATAIFA Edit

 Mimbari ya msikiti nchini Israel ilio na kipaza sauti      


 Mimbari ya msikiti nchini Israel ilio na kipaza sauti 

Kulikuwa na hisia kali katika bunge la Israel siku ya Jumatano wakati lilipopitisha sheria kuzuia vipaza sauti miongoni mwa taasisi za kidini. 

Matoleo mawili ya ''muswada wa Muezzin'' ambao ungeathiri wito wa ibada miongoni mwa Waislamu 'Adhan' ulisomwa kwa mara ya kwanza na kupitishwa na wachache.

Baadhi ya wabunge Waarabu walizikatakata baadhi ya nakala za muswada huo wakati wa mjadala.

Muswada huo utalazimika kusomwa kwa mara nyengine na kupitishwa kabla ya kufanywa sheria.

Toleo moja la muswada huo linapiga marufuku taasisi zote za kidini kutumia vipaza sauti kati ya saa tano na saa moja.

Toleo jingine linapiga marufuku vipaza sauti vinavyoonekana kuwa na kelele zaidi muda wowote wa siku.

Ni marekebisho ya muswada ulioidhinishwa na baraza la mawaziri la Benjamin Netanyahu mnamo mwezi Novemba.

Bwana Netanyahu alisema kuwa amepokea malalamishi kadhaa utoka katika jamii zote za Israel kuhusu kelele na matatizo wanayopata kutokana na kelele hizo zinazotoka katika vipaza sauti.


  
 Mbunge aliyekasirishwa na muswada huo na kuamua kuukatakata
Mbunge aliyekasirishwa na muswada huo na kuamua kuukatakata
Mmoja ya watu wanaopigia debe muswada huo Motti Yogev wa chama cha Jewish Home Party alisema siku ya Jumatano kwamba ni muswada unaolenga kuwasaidia raia kupumzika

''Hatuna nia ya kuwaumiza wafuasi wa dini yoyote'', aliongezea.

Wakosoaji wa muswada huo wanasema kuwa unakandamiza uhuru wa kuabudu.

''Sauti ya ''Adhan'' haijawahi kusababisha uchafuzi wowote wa mazingira.Ni mojawapo ya tamaduni za dini ya kiislamu na hatujawahi kingilia sherehe yoyote ya kidini inayohusu Judaism. Vitendo vyenu ni vya kibaguzi'' ,alionya Ahmed Tibi wa chama cha Joint List alliance chenye Waarabu wengi.

''Hatua hii inalenga Uislamu'', aliongezea.
Ayman Odeh kiongozi wa muungano huo alifurushwa nje baada ya kukatakata nakala ya muswada huo.

Netanyahu ataka sauti za 'adhan' kupunguzwa misikitini

Raia wa Kiarabu nchini Israel wanaojulikana kama Waarabu Waisraeli ni kizazi cha Wapalestina 160,000 waliosalia baada ya taifa la Israel kubuniwa 1984.

Wao ni asilimia 20 ya idadi ya Waisraeli .
Asilimia themanini ya Waisraeli Waarabu ni Waislamu na waliosalia wamegawanyika sawa kati ya Wakristo na Druze
chanzo 
bbcswahili
Share on Facebook Share on Twitter Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

RELATED POSTS

    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment

Newer Post Older Post Home
Subscribe to: Post Comments ( Atom )

VIDEO: MBOWE AKIZUNGUMZIA SAKATA DAWA ZA KULEVYA



ZILIZOSOMWA ZAID WIKI HII

  • Majibu ya Jeshi la Polisi Makao Makuu kuhusu tuhuma za Rushwa dhidi ya Kamanda Sirro
    Jeshi la polisi nchini limesema litafanya uchunguzi wa tuhuma za rushwa dhidi ya Kamishna wa Polisi Kanda Maa...
  • VIDEO: Mbunge wa zamani Idd Azan alivyofika kituo cha polisi kati kutii wito wa Makonda
    Baada ya Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kutangaza awamu ya pili ...
  • Wabunge wa upinzani Walivyosusa na kutoka nje kisa kukamatwa kwa Tundu Lissu
    Wabunge wote wa vyama vya upinzani waliokuwa bungeni katika kikao kinachoendelea jioni hii wametoka nje ya ...
  • Mwalimu Mkuu akamatwa na TAKUKURU akiomba rushwa ya ngono
    ...
  • UDA Yazikwa Rasmi.....Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Yavunja Mkataba
    Tuesday, May 10, 2016 Hatimaye  uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, umevunja mkataba wa uweke...
  • MWIGULU, UMMY MWALIMU WATE MBELEA MACHINJIO YA VINGUNGUTI NA KUJIONEA HALI HALISI YA MAZINGIRA
    Mgakuzi wa Vyakula kutoka Mamlaka a Chakula na Dawa, Dk Itikija Mwanga (kushoto) akitoa maelezo kwa  Waziri wa Kilimo,Mifugo na ...
  • Picha: Mapokezi ya Diamond, Familia yake na Team yake Mjini KISUMU
    Nkupamah media:
  • Taarifa rasmi ya Serikali kuhusu kesi ya kupinga Kanuni za Mitandaoni na maelekezo mahsusi kuhusu usajili wa mitandao ya kijamii.
  • Barcelona Kuendeleza Ushindi Dhidi Ya Deportivo Kesho?
    Baada ya mchezo wa katika ya wiki dhidi ya PSG ,FC Barcelona hapo kesho itakua na kibarua kizito pale itakaposafiri na kuelekea Galicia...
  • TANZANIA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO WA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII AFRIKA MASHARIKI NA KATI (ECASSA)
    nkupamah media:  
Powered by Blogger.

GLOBU RAFIKI

  • Bongo Blogs - Blog ya Taifa
    Majina ya Blog Zinazoanzia na Herufi ya V - *1. VOA Sauti ya America * www.voaswahili.com *2. Vijimambo* lukemusicfactory.blogspot.com
    1 year ago
  • DEWJIBLOG
    Nhà Cái VF555 Nhiều Chương Trình Khuyến Mãi VF555 Tặng 128K - Nhà cái VF555 Tặng 128K không chỉ nổi tiếng với sự uy tín mà còn là điểm đến lý tưởng cho những người yêu thích các trò chơi cá cược. Với nhiều chương trìn...
    2 years ago
  • Chadema Blog
    Hotuba ya Lissu; azungumzia kukoma Ubunge, atangaza hatua zinazofuata - Kuangalia unaweza kugonga hapo chini https://youtu.be/PpwHmbRrKoI
    7 years ago
  • Home
  • Portfolio
  • Gallery
  • Archive
    • Dec 2012
    • Jan 2013
    • May 2014
    • Feb 2015
  • Blog
  • About
  • Contact
  • Home

Flickr Images

Labels

  • BURUDANI
  • JAMII
  • KIMATAIFA
  • KITAIFA
  • MAGAZETI
  • MICHEZO
  • SIASA
  • UCHUMI

co


Copyright © 2014 Tz News Blog
Blogger Templates