Mkuu wa mkoa kilimanjaro Anna Elisha Mgwira akiongea jambo la shukrani mara baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam June 6, 2017
Magufuli amemshahuri asikubali kuyumbishwa na mtu yeyote katika majukumu yake katika kuwahudumia wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro.
“Mimi huwa siteui watu hivi hivi, huwa naangalia uwezo wa mtu, na wewe nimekuchunguza na nimejiridhisha kuwa una uwezo wa kuwatumikia wananchi, nenda kachape kazi, kawaondolee kero wananchi wa Kilimanjaro, wapo watu watakaokusema na wengine watakuonea wivu, wewe kachape kazi” amesema Rais Magufuli.
Kwa upande wake Anna Mghwira, amemshukuru Rais Magufuli, kwa kumteua kuwa mkuu wa mkoa na kusema kuwa anaamini kuwa hakuna upinzani usiyopenda maendeleo na yeye si mpinzani wa maendeleo.
“Ninasema hii ni heshima kwa Taifa letu, ni heshima kwa umoja wa nchi yetu, ni heshima kwa siasa za umoja wa nchi yetu, kumekuwa na minong’ono mingi sana kuwa Rais analeta nini, kuteua watu wanaitwa wapinzani, mimi sio mpinzani wa maendeleo” amesema Mghwira.Facebook