Hivi karibuni kumesikika Uvumi kuwa Sportpesa wanataka kuzipeleka Klabu za Simba, Yanga na Singida United nchini Uingereza kujiandaa na Msimu ujao wa ligi kuu Tanzania bara.
Mkurugenzi wa sportpesa Abbas Tarimba amekiri kuwepo kwa mpango huo na kuongozea kuwa klabu hizo zitakwenda nchi mbalimbali za Ulaya.Mkurugenzi huyo aliyesema hayo wakati wa mahojiano tulipokutana nae kwenye ibada ya mwisho ya kuaga mwili wa marehemu mke wa Waziri Mwakyembe, Linah Mwakyembe aliyefariki wiki iliyopita.



0 comments :
Post a Comment