Korea Kaskazini Yapiga Marufuku Sherehe Za Krismasi

Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un amepiga marufuku mikusanyiko inayoashiria kusherehekea sikukuu ya Krismasi kama vile inayohusu unywaji na uimbaji.
Ametaka wananchi kutosherehekea sikukuu hiyo na wanaopenda kufanya hivyo, waitumie Desemba 24 kusherehekea siku ya kuzaliwa kwa bibi yake aliyezaliwa siku kama hiyo mwaka 1919.
Kiongozi huyo ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha vinadhibiti mikusanyiko yote ambayo inaendana na maadhimisho ya Krismasi.
“Ni marufuku watu kukusanyika na kufanya mambo kama ya unywaji au kuimba katika sikukuu ya Krismasi,” chanzo kimoja cha habari kimenukuu taarifa ya kiongozi huyo.
Kim Jong Un amekuwa akichukua hatua kuzua kuenea kwa utamaduni kwa kigeni na amedhibiti vyombo vya habari kutotangaza taarifa zozote zinazoienzi sikukuu hiyo kama hatua ya kupiga marufuku Krismasi.
Ingawa sikukuu ya Krismasi si tukio kubwa nchini humo, lakini baadhi ya wananchi wamekuwa wakiisherekea na kufuata misingi ya Kikristo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment