Mwigulu:Wapinzani Wameogopa Kushiriki Uchaguzi

Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba amezindua kampeni za Chama Cha Mapinduzi katika uchaguzi mdogo jimbo la Longido unaotarajiwa kufanyika Januari 13, 2018 na kusema kwamba wapinzani wameogopa kushiriki kwa sababu wataachwa mbali sana.



Akizindua kampeni hizo, Mwigulu amewataka wananchi wa jimbo la Longido kumchagua mgombea wa CCM, Dk. Steven Kiruswa awe mbunge wao kutekeleza ilani ya chama mapinduzi kwa kuwaletea maendeleo ambayo wameyakosa kwa miaka miwili.



Mwigulu amesema wapinzani wameogopa kuwa wataachwa mbali k baada ya kupima uitikio wa wananchi ambao wanakubali kazi za Rais John Magufuli na serikali ya Chama Cha Mapinduzi ambayo inatekeleza ilani ya CCM kwa vitendo na wananchi wanaona.



Aidha amewahakikishia wananchi wajitokeze siku ya kupiga kura kwani usalama ni wa uhakika wakati wa kupiga kura.​
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment