Ripoti Ya Uchunguzi Kampuni Ya Airtel Yatua Kwa Rais Magufuli


Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amewasilisha kwa Rais John Magufuli taarifa ya kamati aliyoiunda kuchunguza umiliki wa kampuni ya simu Airtel na kueleza jinsi Serikali ilivyoingizwa mkenge.

Taarifa hiyo imewasilishwa  baada ya Rais Magufuli kutoa agizo la kufanyika hivyo Desemba 20 mwaka jana.

Baada ya kuwasilisha taarifa hiyo, Dk Mpango alisema Serikali imejiridhisha kuwa ubinafsishaji wa Shirika la Simu Tanzania (TTCL) kwenda Celtel, baadaye kuhamishiwa Zain na sasa Airtel ulifanyika kwa ukiukwaji mkubwa wa sheria, kanuni na taratibu.

Kufuatia ukiukwaji huo Dk Mpango amesema Serikali inayomiliki asilimia 40 ya hisa za kampuni ya Airtel imeamua kufanya mazungumzo na kampuni ya Airtel inayomiliki asilimia 60 ya hisa ili nchi iweze kupata haki yake.

“Lakini niwaambie Watanzania yale ambayo tumeyaona ni machafu sana, ni mambo ya hovyo kabisa, nchi yetu kwa kifupi tuliingizwa mkenge, ni fedha nyingi zimepotea kwa hiyo sisi katika majadiliano haya lengo letu litakuwa ni kuhakikisha Watanzania wanapata haki yao,” alisema Dk Mpango.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment