Chopa ya Chadema yazua mvutano uchaguzi mdogo Kalenga



Chopa ya Chadema ikiwa angani tayari kupeleka viongozi kwenye mikutano ya uchaguzi. Picha na Maktaba 
Na Geofrey
Nyang’oro na Zainab Maeda, Mwananch
Kwa ufupi
  • Polisi waitaka Chadema kutotumia siku ya uchaguzi kwa madai kuwa itavuruga wanapigakura.
SHARE THIS STORY

0
Sha

Kalenga. Polisi katika Mkoa wa Iringa, imepiga marufuku matumuzi ya helkopta siku ya uchaguzi mdogo wa Kalenga, kwa madai kuwa kufanya hivyo ni sawa na kupiga kampeni.
Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Ramadhani Mungi alitoa kauli hiyo jana wakati akitoa taarifa ya hali ya usalama tangu kampeni zilipoanza hadi sasa kwa vyombo vya habari.
Mungi alisema siku ya uchaguzi siyo siku ya kampeni na kwamba polisi hawatakubali kuona vitendo vya kampeni vikionekana miongoni mwa wakazi wa Kalenga ikiwamo helkopta kutumika katika jimbo hilo na watu waliosafiri kutoka mikoa mbalimbali kwa kisingizio cha kulinda kura.
“Sasa nataka niwaeleze kuwa sheria iko wazi. Siku ya uchaguzi si siku ya kampeni. Hatutaki kuona helkopta za vyama vyote zenye kuashiria kufanya kampeni. Kila kituo cha kupigia kura kitakuwa na wakala wa chama kinachoshiriki katika uchaguzi huo na hao ndiyo wawakilishi wa chama hicho na walinzi halali wa uchaguzi ni polisi”alisema Mungi na kuongeza:
“Hatutaki kuona walinzi wa chama chochote katika Jimbo la Kalenga. Jukumu la kulinda uchaguzi, maisha na mali ya wana Kalenga ni la polisi, hatutaki kuona watu wasiokuwa na shughuli maalumu wanapitapita katika maeneo ya kupigia kura”alisema.
Tume wazungumzia
Wakati Mungi akitoa kauli hiyo, Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) ilishindwa kutoa jibu la moja kwa moja kama helkopta hiyo itatakiwa kutumika ama la, hali iliyosababisha maswali mengi kutoka kwa waandishi wa habari.
Majibu ya Tume yalitolewa katika mkutano ulioitishwa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Mstaafu Damian Lubava ambaye kabla ya yeye kutoa ufafanuzi alitaka wajumbe wenzake kutolea majibu.
Akijibu swali la matumizi ya Chopa liloulizwa katika mkutano huo, Jaji Mstaafu John Mkwawa alisema “Matumizi ya vyombo vya usafiri tume haijakataza, ila mtu hapaswi kutumia kitu chochote kinacholeta hali isiyo nzuri na kusababisha usumbufu, chopa inaweza kusababisha kelele”alisema.
Naye Profesa Amon Chaligha alisema matumizi ya helkopta ni sehemu ya kampeni na kuongeza kuwa kimsingi isingeruhusiwa kutumika siku ya kampeni.
Akifafanua, Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damian Lubuva alisema vyombo vyote vya usafiri vinaruhusiwa kutumika siku ya kampeni, lakini kwa namna ambavyo vitatofautina na namna vilivyokuwa vikitumika wakati wa kampeni.
“Kama Helkopta itapangiwa utaratibu utakaotofautiana na ule uliotumika wakati wa kampeni,…kumpelekea mtu kuruka kutoka uwanja wa ndege na kwenda eneo husika bila ya kuathiri kuonesha mazingira ya kupiga kampeni hapo sawa, lakini sheria inasema siku ya uchaguzi siyo siku ya kampeni” alisema.
1 | 2 | 3 | 4 Next
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment