Majibu ya mgombea wa CHADEMA kwa mgombea wa CUF-JIMBO LA CHALINZE


MAJIBU/MAELEZO YA PINGAMIZI LILILOWEKWA NA BWANA FABIAN L.SKAUKI DHIDI YANGU MIMI MATAYO M.TORONGEY MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA CHALINZE KUPITIA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA)
.

UTANGULIZI
Kwa mujibu wa ibara ya 67 (1) ya Katiba ya Jamhuri Muungano wa Tanzania (1977) inaeleza wazi kuwa ili mtu ateuliwe kuwa mgombea ubunge ni lazima awe na sifa zifuatazo;
(i)-Awe raia wa Tanzania
(ii)-Awe ametimiza umri wa miaka ishirini na moja
(iii)-Awe anajua kusoma na kuandika kwa Kiswahili au Kiingereza
(iv)-Awe ni mwanachama na ni mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa
(v)-Awe hajatiwa hatiani na mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa kodi yoyote ya Serikali katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya Uchaguzi.
Aidha, Kwa mujibu wa Ibara ya 67 (2) na -(3) -ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania 1977; hata kama mtu ana sifa zote za kugombea -hataruhusiwa kugombea Ubunge kama :
(i)-Ni raia wa nchi nyingine; au
(ii)-Kwa mujibu wa Sheria iliyotumika katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imethibitishwa rasmi kwamba mtu huyo ana ugonjwa wa akili; au
(iii)--Amehukumiwa na Mahakama yoyote katika Jamhuri ya Muungano na kupewa adhabu ya kifo au ya kufungwa gerezani kwa muda usiozidi miezi sita kwa kukutwa na hatia ya kosa lolote, vyovyote linavyoitwa, linaloambatana na utovu wa uaminifu; au
(iv)-Katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya Uchaguzi Mkuu amepata kuhukumiwa na kupewa adhabu ya kifungo kwa kosa linaloambatana na utovu wa uaminifu au kwa kuvunja sheria ya maadili ya viongozi wa Umma; au
(v)-Siyo mwanachama na siyo Mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa; au
(vi)-Ikiwa mtu huyo ana maslahi yoyote katika mikataba na serikali ya Jamhuri ya Muungano au serikali ya mapinduzi Zanzibar wa aina yoyote aliyowekewa miiko maalumu kwa mujibu washeria iliyotungwa na Bunge, na iwapo amekiuka miiko hiyo; au
(vii)-Ameshika madaraka ya Afisa Mwandamizi katika utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano, isipokuwa madaraka ambayo Rais anaweza au anatakiwa kukabidhi kwa Mbunge kwa Mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano, au sheria iliyotungwa na Bunge; au
(viii)-Kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge inayoshughulikia makosa yanayohusika na uchaguzi wa aina yoyote, mtu huyo amezuiliwa kuandikishwa kama Mpiga kura au kupiga kura katika uchaguzi wa Wabunge.
(ix)-Ni mgombea Urais /Umakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Aidha, kwa mujibu wa masharti kwa vyama vya siasa na wagombea uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani yaliyotolewa na Tume ya Taifa ya uchaguzi kifungu cha 5.3 kimeweka masharti ya Uteuzi wa Mgombea Ubunge na kuweka kama ifuatavyo;
(i)-Awe amedhaminiwa na wapiga kura wasiopungua ishirini na tano waliojiandikisha kupiga kura katika Jimbo hilo.
(ii)-Mgombea haruhusiwi kujidhamini yeye mwenyewe
(iii)-Awe na dhamana ya shilingi 50,000/=
(iv)-Awe ametoa tamko la kisheria mbele ya hakimu kwamba anazo sifa zinazotakiwa ili kugombea Ubunge
Vilevile, kwa mujibu wa masharti kwa vyama vya siasa na wagombea uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani yaliyotolewa na Tume ya Taifa ya uchaguzi kifungu cha 6.0 kimeweka utaratibu wa Pingamizi dhidi ya uteuzi wa Mgombea Ubunge:
Na Kifungu cha 6.3, kimeweka sababu za kuweka Pingamizi kuwa ni:
(i)-Maelezo yaliyopo katika fomu ya uteuzi hayatoshi kumtambulisha Mgombea;
(ii)-Fomu ya Uteuzi haitimizi au haikuwasilishwa kwa mujibu wa masharti yaliyowekwa na sharia;
(iii)--Kutokana na maelezo yaliyoandikwa katika fomu ya uteuzi ni dhahiri kwamba Mgombea uchaguzi hana sifa zinazotakiwa;
(iv)-Uthibitisho wa Msimamizi wa Uchaguzi unaopaswa kutolewa haukutolewa; (v)-Mgombea hana sifa zote zinazotakiwa;
(vi)-Hakuna uthibitisho kuwa Mgombea amelipa dhamana ya shilingi elfu hamsini (50,000/=); na
(vii)-Hakuna picha ya Mgombea.
(viii)-Mgombea hakujaza fomu Na.10 kuthibisha kuwa ataheshimu na kutekeleza maadili ya Uchaguzi.
Baada ya utangulizi huo hapo juu ambao unaonyesha dhahiri kuwa hapakuwa na sababu yoyote ya mimi kuwekewa pingamizi na Mgombea ubunge wa Chama cha CUF, kwani hakufuata masharti ya Katiba, Sheria na maelekezo yaliyotolewa na Tume ya Taifa ya uchaguzi kwetu kama wagombea, kwani aliamua kutunga mambo ambayo yapo nje ya utaratibu na hayakidhi haja, hayakufuata Katiba, matakwa ya kisheria na hata maelekezo yaliyotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.


Nayasema yote haya kutokana na ukweli kuwa mimi nimekidhi sifa zote za kuwa Mgombea Ubunge na nimetimiza masharti yote yaliyowekwa kwa mujibu wa Katiba na Sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kutokana nabarua yako ya tarehe -13 Machi, 2014 yenye kumbukumbu namba HWB/E.50/21/76-nalazimika kujibu pingamizi hilo kwa mujibu wa kifungu cha sheria ya Uchaguzi sura Na.343 kifungu Na.40 (5)-kuhusu pingamizi,-hata kama halina nguvu kwa mujibu wa katiba, sheria na maelekezo ya Tume ya taifa ya uchaguzi hoja kwa hoja kama ifuatayvo. -

ENDELEA.......

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment