Na Mussa Juma, Jumatatu,Marchi24 2014 saa 11:55 AM
Kwa ufupi
Umoja huu unaundwa na wajumbe kutoka vyama vya
upinzani na baadhi ya wawakilishi wa makundi yaliyoteuliwa na Rais
Jakaya Kikwete na baadhi ya wabunge wa CCM.
Julius Mtatilo ni katibu wa muda wa kundi hilo.
Katika mahojiano maalumu na Mwananchi, Mtatiro anaeleza mambo kadhaa
yanayohusu umoja huo kama ifuatavyo;
Swali: Katika siku za karibuni Ukawa ni moja ya
makundi ambayo yamekuwa yakitajwa sana kwenye Mchakato wa Katiba Mpya.
Je, nini maana yake na ulianza lini?
Jibu: Ukawa ni kifupi cha Umoja wa Kutetea Hoja za
Wananchi zilizopo kwenye Rasimu ya Katiba ambayo imewasilishwa bungeni
na Jaji Joseph Warioba.
Swali: Umoja huu umeanzishwa lini na kwanini ulianzishwa?
Jibu: Ukawa ulianzishwa mara tu baada ya kufika
bungeni na kuona wenzetu CCM wana misimamo yao kuhusu Rasimu ya Katiba
na wamekuwa wakikutana na kutoa maoni tofauti na Rasimu ya Katiba.
Tulipobaini hilo, tukaona ni busara kuanzisha Ukawa ili kutetea maoni ya
wananchi katika rasimu.
Swali: Je, umoja huu una jumla ya wanachama wangapi?
Jibu: Umoja huu ulianzishwa ukiwa na wanachama 203
na hadi sasa tuna jumla ya wanachama 286, kati yao kuna wabunge wanne
wa CCM na tunatarajia wanachama kuongezeka zaidi.
Swali: Je, umoja huu unaongozwa na kina nani, baada ya kupata wazo na kuanzishwa?
Jibu: Ukawa ulichagua viongozi wa muda. Mwenyekiti
ni James Mbatia na mimi ni katibu. Pia kuna wenyeviti wenza kama
Profesa Ibrahim Lipumba na Freeman Mbowe na yupo Tundu Lissu na wengine
wengi.
Swali: Je, mna mpango wa kufanya uchaguzi ili kuwa na viongozi wa kudumu hadi mwisho wa Bunge hili maalumu?
0 comments :
Post a Comment