Hatutakubali kuburuzwa bungeni

Na Mussa Juma,  Jumatatu,Marchi24  2014  saa 11:55 AM

Kwa ufupi
Katibu wa Ukawa, Julius Mtatiro amesema umoja huo una mpango wa kufanya uchaguzi kwa ajili ya kupata viongozi wa kudumu

Dodoma.Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ni moja ya makundi ambayo yamekuwa na sauti kubwa katika Bunge la Katiba linaloendelea mjini Dodoma.
Umoja huu unaundwa na wajumbe kutoka vyama vya upinzani na baadhi ya wawakilishi wa makundi yaliyoteuliwa na Rais Jakaya Kikwete na baadhi ya wabunge wa CCM.
Julius Mtatilo ni katibu wa muda wa kundi hilo. Katika mahojiano maalumu na Mwananchi, Mtatiro anaeleza mambo kadhaa yanayohusu umoja huo kama ifuatavyo;
Swali: Katika siku za karibuni Ukawa ni moja ya makundi ambayo yamekuwa yakitajwa sana kwenye Mchakato wa Katiba Mpya. Je, nini maana yake na ulianza lini?
Jibu: Ukawa ni kifupi cha Umoja wa Kutetea Hoja za Wananchi zilizopo kwenye Rasimu ya Katiba ambayo imewasilishwa bungeni na Jaji Joseph Warioba.
Swali: Umoja huu umeanzishwa lini na kwanini ulianzishwa?
Jibu: Ukawa ulianzishwa mara tu baada ya kufika bungeni na kuona wenzetu CCM wana misimamo yao kuhusu Rasimu ya Katiba na wamekuwa wakikutana na kutoa maoni tofauti na Rasimu ya Katiba. Tulipobaini hilo, tukaona ni busara kuanzisha Ukawa ili kutetea maoni ya wananchi katika rasimu.
Swali: Je, umoja huu una jumla ya wanachama wangapi?
Jibu: Umoja huu ulianzishwa ukiwa na wanachama 203 na hadi sasa tuna jumla ya wanachama 286, kati yao kuna wabunge wanne wa CCM na tunatarajia wanachama kuongezeka zaidi.
Swali: Je, umoja huu unaongozwa na kina nani, baada ya kupata wazo na kuanzishwa?
Jibu: Ukawa ulichagua viongozi wa muda. Mwenyekiti ni James Mbatia na mimi ni katibu. Pia kuna wenyeviti wenza kama Profesa Ibrahim Lipumba na Freeman Mbowe na yupo Tundu Lissu na wengine wengi.
Swali: Je, mna mpango wa kufanya uchaguzi ili kuwa na viongozi wa kudumu hadi mwisho wa Bunge hili maalumu?
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment