Mgombea Urais wa 40 CCM Achukua Fomu ya Kugombea Urais

Friday, June 26, 2015

Nkupamah blog

Hellena Elinewinga, Mtaalam wa masuala ya utafiti, amekuwa kada wa 40 wa CCM kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa na chama hicho, kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akizungumzia hatua hiyo baada ya kuchukua fomu hiyo jana, Hellena alisema ameamua kujitosa katika kinuanganyiro hicho, kwa kuwa anachukizwa na baadhi ya aina ya viongozi wanaoshindwa kutoa huduma stahiki kwa watanzania na kujinufaisha wenyewe.

Hellena alikabidhiwa fomu hiyo jana, na Khatibu, saa 7:20 mchana huku akisisitiza kwamba kama chama chake kitamteua kugombea kiti hicho, atahakikisha viongozi wanaokwamisha mchakato wa maendeleo au kulihujumu taifa, wanahukumiwa adhabu ya kifo kutokana na mchango mbovu walioutoa.

Mgombea huyo anayefanya kazi na Asasi za Kiraia na Taasisi za Kilimo katika mikoa ya Kanda ya Kaskazini; ni mkazi wa Tarafa ya Masama, Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro.

Hellena (40), sasa anakuwa mwanamke wa sita kujitosa kuomba ridhaa ya chama chake. Wengine ni Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Asha- Rose Migiro; Naibu Waziri wa zamani wa Fedha na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Monica Mbega; Balozi Amina Salum Ali; Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu, Dk. Mwele Malecela na Ofisa Maendeleo ya Jamii, Ritha Ngowi.
Nkupamah blog
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment