AFISA WA PCCB AFA KATIKA AJALI, ALIKUWA ANAWAHI KUTANGAZA NIA YA KUWANIA UBUNGE HUKO NJOMBE

AFISA wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, PCCB, Conrad Mtenga (53) maarufu kama Chillangamsafa amefariki katika ajali kwenye barabara kuu ya Mbeya-Iringa.

Watu wawili wamejeruhjiwa kwenye ajali hiyo iliyotokea eneo la Tanangozi, baada ya gari dogo aina ya Nissan Patrol, mali ya AfriCarriers, kugongana uso kwa uso na Lori aina ya Scania.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Pudenciana Protas alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 8:30 mchana eneo la Tanangozi barabara kuu ya Iringa- Mbeya
Kamanda Ptotas alisema kuwa gari hiyo yenye namba za usajili T.291 BNK aina ya Nisan Patrol mali ya Africafrie’s Ltd ya Jijini Dar es salaam ilikuwa ikiendeshwa na Conrad Mtenga (53) maarufu kwa jina la Chillangamsafa ambaye ni mfanyakazi wa PCCB na mkazi wa chunya. Alisema kuwa gari hiyo iligongana na gari aina ya Scania yenye namba T.783 ATQ ambayo ilikuwa ikiendeshwa na dereva Henry Lulandala ( 35) na kusababisha kifo cha dereva huyo.
Majeruhi walitajwan kuwa ni pamoja na Baraka Zakayo na Rebeca Mtenga, wote wamelazwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa. Kaimu kamanda huyo wa polisi alisema, uchunguzi wa awali unaonyesha derive wa gari dogo alihama kutoka upande wake na kumfuata mwenye gari kubwa na hivyo kugongana uso kwa uso.
Marehemu Conrad Mtenga
Mabaki ya gari dogo aina ya Nissan Patrol, baada ya ajali hiyo -K-Vis Blog
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment