……………………………………..
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania
imewataka wananchi wenye malalamiko kuhusu vitendo vya rushwa
mahakamani kutoa ushirikiano ili kuweza kutafuta ufumbuzi wa tatizo
hilo.
Hayo yalisemwa katika taarifa
kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo jijini Dar es salaam na Afisa
Habari Mary Gwera wa Mahakama hiyo kufuatia gazeti moja la hapa nchini
la Julai 21 mwaka huu kupitia makala yenye kichwa cha habari “Mtandao
wa rushwa Mahakamani huu hapa” .
Taarifa hiyo imeeleza kuwa,
baada ya kufanya uchunguzi juu ya kesi zilizoandikwa katika makala
hiyo Mahakama haikuweza kupata maelezo sahihi kuhusu kesi mbalimbali
za watu wenye malalamiko hayo ambao ni Muhidini Nguluma ,Kuruthum
Majjid, Abadallah Majata, Halima Abdan, Claudiana Mbazigwa Mpondela
na Laizer Kaanan.
“Ili kuondoa kero
zilizobainishwa katika gazeti la Mwananchi , mahakama inatoa rai kwa
gazeti la Mwananchi au mtu yoyote mwenye taarifa sahihi kuipatia
ushirikiano ili kupata namba za simu za kesi zilizolalamikiwa na
mahakama zilikofunguliwa,” ilisema taarifa hiyo.
Aidha mahakama hiyo imeomba
wale wote waliotajwa katika makala hiyo wafike Makao Makuu ya Mahakama,
Mahakama ya Rufani ya Tanzania, Namba 11409 Kivukoni Front waonane na
Mkurugenzi Msaidizi wa Malalamiko katika Idara ya Ukaguzi wa Huduma za
Mahakama na Maadili ili watatuliwe kero zao.
Mahakama hiyo inasisitiza kwamba imeweka namba za simu 0752–500 400. mitandao ya kijamii, WhatsApp, na barua pepe info@judiciary. go.tz) ili wananchi na wadau mbalimbali waweze kutoa malalamiko yao, maoni na mapendekezo.


0 comments :
Post a Comment