WIZARA YA NISHATI NA MADINI YAANZA MAFUNZO KUHUSU HUDUMA ZA LESENI ZA MADINI KWA NJIA YA MTANDAO KATIKA KANDA YA KASKAZINI

ma1
Mtaalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Kitengo cha Leseni Charles Gombe akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kwenye Ofisi ya Afisa Madini Mkazi – Kilimanjaro kabla  ya  kuanza kwa uendeshaji wa mafunzo ya huduma  za leseni kwa njia ya mtandao.  Mafunzo hayo yanahusisha wachimbaji wa madini lengo likiwa ni kuwapa uelewa wa matumizi ya huduma za leseni kwa njia ya mtandao
ma2
Mtaalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Kitengo cha Leseni Charles Gombe akielezea mikakati ya  Wizara katika  uboreshaji wa huduma za leseni kwa wachimbaji wa madini (hawapo pichani) katika mafunzo yaliyofanyika  wilayani Same mkoani Kilimanjaro
ma3
Baadhi ya wachimbaji wa madini  kutoka wilaya ya  Same mkoani Kilimanjaro wakifuatilia kwa makini mada  zilizokuwa zinawasilishwa na wataalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini (hawapo pichani)
ma4
Mmoja wa wachimbaji wa madini kutoka  wilayani Same, mkoani Kilimanjaro Richard Mbwambo akiuliza swali katika mafunzo hayo
ma5
Afisa Madini Mkazi, Mkoa wa Kilimanjaro, Fatuma Kyando akielezea  sheria na kanuni za uchimbaji wa madini  nchini katika mafunzo hayo
ma6
Mmoja wa wachimbaji wadogo, Naamin Samuel kutoka kampuni ya Kivoroi na Ndarauoi akiuliza swali katika mafunzo hayo
ma7
Wataalam kutoka  Wizara ya Nishati na Madini ( waliokaa mbele) wakiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo hayo  waliosimama nyuma.
ma8
Baadhi  ya watoto kutoka wilayani Same mkoani Kilimanjaro wakipozi katika picha ya pamoja mbele ya  gari la matangazo la Wizara ya Nishati na Madini lililokuwa linatumika wakati wa zoezi la uhamasishaji  wa matumizi  ya huduma za leseni  za madini kwa njia ya mtandao.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment