Hii ndio Historia na Asili ya Mji wa Tanga.???

Mji wa Tanga ni Mji Mkuu wa Mkoa wa Tanga uliopo ufukweni mwa Bahari ya Hindi. Tanga ina bandari kubwa kabisa katika sehemu ya kaskazini mwa Tanzania. Njia ya reli kwenda Mji wa Moshi inaanza hapa.
Jina hili la mji wa Tanga lilitokana neno la Kiajemi lenye maana nne tofauti ambazo ni: Iliyo nyooka; 
Bonde lenye rutuba; 
Barabara upande wa mto na 
Shamba juu ya mlima.
Neno hilohilo la Tanga kwa kabila la Kibondei ambalo ni wenyeji wa mkoa huo lina maana ya shamba, wao hulitamka N'tanga.
Tanga insaemekana imeanzishwa na wafanyabiashara Waajemi katika karne ya 14 KK. Mji wa Tanga haukupata umuhimu kama mji wa jirani ya Mombasa. Tarihi ya Pate inasema ya kwamba kabla ya kuja kwa Wareno., Pia Pate iliwahi kutawala Lindi kwa muda fulani.
Katika karne ya 19 KK, Tanga ilikuwa chini ya utawala wa Omani na Zanzibar. Misafara ya biashara imeanzishwa hapa kwenda bara. Kutokana na bandari yake nzuri ya kiasili Tanga ilikua sana wakati wa ukoloni wa Wajerumani waliojenga bandari ya kisasa pamoja na reli kwenda Moshi. Reli iliwezesha kilimo kwa ajili ya soko la dunia na Tanga ikawa bandari kuu kwa ajili ya katani na kahawa. Baada ya Uingereza kuchukua utawala wa Afrika ya Mashariki ya Kijerumani, reli ya Tanga-Moshi iliunganishwa na ile ya kati hivyo ikawa na njia kwenda Daressalaam pia. 
Wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia Tanga iliona mapigano makali tar. 3 - 5 Novemba 1914. Jaribio la Uingereza kuvamia Tanga kwa kikosi cha maaskari 8000 Waingereza na Wahindi kutoka meli kwenye Bahari Hindi Lilishindwa vibaya na Jeshi la Ulinzi wa Kijerumani chini ya uongozi wa Paul von Lettow-Vorbeck.
Mwaka 1922 "Tanganyika Territory African Civil Services Association" (TAA) iliundwa Tanga ambayo ilikuwa shirika ya kwanza ya Kiafrika yenye shabaha za kisiasa.
Kutokana na kupanuka kwa bandari ya Dar-es-salaam, umuhimu wa bandari ya Tanga umerudi nyuma.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment