MABONDIA KUPIMA UZITO IJUMAA KUPIGANA JUMAMOSI KARIAKOO UHURU WASICHANA

Bondia Ibrahimu Class ‘King Class Mawe
Bondia Ally Mulo
……………………………………………………………..
MABONDIA Ibrahimu Class ‘King Class Mawe’ na Ally Mulo watapima uzito siku ya ijumaa kwa ajili ya mpambano wao wa jumamosi utakaofanyika katika viwanja vya basketball vilivyopo katika shule ya uhuru wasichana Kariakoo Dar es salaam
Akizungumzia mpambano huo mratibu ambaye pia ni kocha  wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila ‘Super D’ amesema mabondia hao watapima uzito siku ya ijumaa saa tatu asubuhi kwa ajili ya mpambano wao utakaofanyika jumamosi Agosti 22
Mbali na mabondia hao mabondia wengine watakao onyeshana kazi siku hiyo ni Kelvin Majiba atakaepambana na Vicent Mbilinyi wakati Husein Pendeza akioneshana umwamba na Shomari Mirundi na Raymond Mbwago atazidunda na Roger Masawe na mapambano mengine mengi ya mabondia chipukizi
Mabondia hao watapima uzito katika tawi la mashabiki wa Yanga bomba lililopo mtaa wa Ndanda Kariakoo na mpambano wao kufanyika siku ya jumamosi kuanzia saa kumi,  mwisho kabisa utakuwa utakuwa ni mpambano wa  saa kumi na mbili jioni kati ya mabondia Ibrahimu Class ‘King Class Mawe’ na Ally Mulo mpambano huo umepangwa kuanza mapema  ili kila mtu afurahie ngumi hizo na kurudi nyumbani mapema
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment