COSATO CHUMI AMALIZA TATIZO LA VITANDA HOSPITAL YA MAFINGA MJINI

 @nkupamah blog

  Pichani Mbunge wa jimbo la Mafinga mji ni Cotato Chumi akimkabidhi msaada wa vitanda ,magodoro pamoja na vifaa mbalimbali kaimu mganga mkuu wa hospitali ya Mafinga Dk Abdul Msuya juzi
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatiliwa ugawaji wa vifaa hivyo wakati wa makabidhiano
Mbunge wa mafinga mjini Cosato Chumi akikabidhi vifaa hivyo kwa vitendo
Baadhi ya wadau na wanachama wa chama cha mapinduzi ccm walihudhulia tukio hilo 
…………………………………………………………………………………..
 
TATIZO la upungufu wa vitanda katika wodi ya
akina mama na watoto
katika hospitali ya wilaya ya Mufindi mkoani Iringa
ambalo kwa muda mrefu limekuwa chanzo cha msongamano na uwalazimu
baadhi ya wagonjwa kulala sakafuni sasa limepatiwa ufumbuzi baada ya
uongozi wa hospitali hiyo kupokea msaada wa vitanda na vifaa tiba kutoka
kwa mdau wa maendeleo katika sekta ya afya.

Mbunge wa Mafinga Mjini
(CCM) Cosato Chumi alisema kuwa kwa muda mrefu hospitali hiyo ilikuwa ina
upungufu wa vifaa mbalimbali ikiwemo vitanda hali iliyofanya kuandika maandiko
mbalimbali kwa wahisani  wa nje ya nchi ili kuweza kumsaidia kupata
vifaa hivyo .
  
Alisema kuwa umefika
wakati sasa wadau mbalimbali, mifuko ya kijamii na makampuni kujenga utamaduni
wa kusaidia watu wenye mahitaji mbalimbali wakiwemo watoto wanaoishi kwenye
mazingira magumu na wagonjwa hospitalini kwani kufanya hivyo ni sehemu ya
kurudisha kile wanachokitapa kwa jamii.
 
“Unajua afya ni kila
kitu katika maisha ya binadamu hivyo lazima nitekeleze ahadi zangu nilizotoa
wakati wa kampeni na wanachi lazima tufanye kazi kwa kujituma ili tumuunge
mkono rais wetu ambaye anania ya ya kutuletea maendeleo na kuwataka wadau
mbalimbali kusaidia jamii zenye mahitaji na kuacha kutegemea serikali pekee “
alisema
Chumi aliwaomba wananchi
wa jimbo hilo kuunga mkono kwa kufanya kazi kwa nguvu zote ili walete maendeleo
kwa pamoja maana akifanya kazi pekee yake bila wao hawezi kuleta maendeleo
pekee yake.
  
Msaada huo wa vitanda 16 na magodoro 11 na vitu
mbalimbali umetolewa
na taasisi binafsi inayojishughulisha na masuala ya
afya ya nchini Astralia ijulikanayo kama “Rafiki Surgical Mission” kwa
uratibu wa ofisi ya mbunge wa jimbo la Mafinga mjini 
Alisema kuwa msaada huo aliopatiwa  na rafiki zao hawajatoa hata
senti
tano bali huwa marafiki hao wanachangishana fedha na kununua vifaa
hivyo na kisha kuvisafirisha mpaka bandari kavu ambapo hapo ndio hutumia
garama kusafirisha vifaa hivyo mpaka sehemu husika
“Ndugu
zangu nadhani kila mmoja alikuwa akifahamu machungu waliyokuwa wakipata
mama zetu wanapokuja kujifungua kwa kukosa sehemu za
kujifungulia lakini

leo hii msaada huu utatusaidia sana na yoyote atakayeguswa na anaweza
kuja na kuchangia chochote maana mufindi ni yetu sote na mufindi
itajegwa na wanamufindi wenyewe”alisema
Alisema
jambo kubwa lilokuwa likimuumiza kicha kila kukicha ni tatizo la vifaa
katika hospital, elimu  pamoja na tatizo la maji hivyo ni
wakati

wawanamafinga kushikana kwa pamoja katika kusumkuma mbele gurudumu la
maendeleo ili kuendana na kauli mbiu ya sasa ya HAPA NI KAZI TU.
Akipokea msaada
huo kaimu mganga mkuu wa hospitali ya Mafinga dk Abdul Msuya alisema
kuwa msaada wa vitanda hivyo na magodoro na  vifaa
mbalimbali

utakuwa umemaliza kabisa tatizo la vitanda hospitalini hapo licha ya
kukabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo zinaweza kumalizika endapo
kutatokea mdau mwingine kuwasaidi Kwa upande wake katibu wa ccm wilaya
ya Mufindi Jimsoni Muhagama
alimpongeza
mbunge huyo kwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo huku akimwambia kuwa
ni wakati wa kutekeleza kazi kwa vitendo na wala si
maneno kwani

wananchi wanapaswa kutatuliwa kero mbalimbali zinazowakabili badala ya
kupiga porojo zisizo na msingi .
Mhagama
alisema kuwa kila mmoja anapaswa kuwajibika ipasavyo katika nafasi yake
kwani kasi anayokwenda nayo Rais John Magufuli si ya
mchezo bali ni ya

mchaka mchaka na ili nchi iweze kusimama katika mstari ulionyoka kila
mmoja anapaswa kucheza wimbo wa mchaka mchaka
‘’Huuu si
wakati lelemama huu sio wakati mchezo mchezo ni wakati wa uwajibikaji
,hakika Tanzania tumepata kiongozi mchapa kazi tazama sasa
ni siku ya 27

nchi inaongozwa na watu wanne lakini kila sektaa imenyoka na mimi 
nasemaa Magufuli wanyooshe tu kwa kuwa watu walikuwa wakifanya kazi kwa
mazoeya bila ya kuangalia madhara wanayopata
watanzania
swengi
Hata
hivyo Mhgama alisema kuwa kwa kuwa kipindi cha muda mchache nchi inaongozwa
na watu wachache na nchi imesimama haoni sababu ya kuwa na
baraza kubwa

la mawaziri bali Rais Magufuli achague baraza dogo kama
la watu
10 ili kupunguza mzigo kwa serekali yake ya kuwa na mawziri wengi
wasiokuwa na tija  .
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment