KIGALI,Rwanda
Rais PAUL KAGAME wa RWANDA amesema
serikali yake haitapeleka askari wake kwenda kuungana na majeshi ya
Umoja wan chi za AFRIKA yatakayokwenda kulinda amani katika nchi ya
jirani ya
BURUNDI.
Kiongozi huyo ametoa kauli hiyo huku
akiendelea kupinga shutuma kuwa nchi yake imekuwa ikiwapatia silaha
wakimbizi kutoka BURUNDI, ambao ni waasi.
Nchi HAMSINI na NNE wanachama wa Umoja wa AFRIKA, zinatarajia kupeleka askari Elfu tano nchini BURUNDI kwenda kulinda amani.
Hatua hiyo ni kuisaidia nchi ya BURUNDI isiingia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Umoja huo unatarajia kupeleka askari
wake nchini BURUNDI, licha ya upande wa upinzani nchini humo kudai kuwa
hatua hiyo ni uvamizi wa mataifa ya kigeni.
Nchi ya BURUNDI ilijikuta katika ghasia,
baada ya rais wan chi hiyo PIERRE NKURUNZIZA kutangaza nia yake ya
kugombea kiti cha urais kwa muhula wa tatu. Licha ya maandamano ya
wananchi kupinga hatua hiyo NKURUNZINZA aligombea urais mwezi JULY mwaka
huu na kupata tena fursa ya kuiongoza BURUNDI
0 comments :
Post a Comment