Mawaziri na Manaibu Walioteuliwa Juzi Kuapishwa Jumatatu

Nkupamah media

Tarehe 23 Desemba, 2015 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliwateua Mawaziri wanne, Naibu Waziri mmoja na kumhamisha Wizara Waziri mmoja.

Walioteuliwa ni Waziri wa Maliasili na Utalii Profesa Jumanne Maghembe, Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge, Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Dkt. Joyce Ndalichako na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mheshimiwa Hamad Yusuf Masauni.

Rais Magufuli pia alifanya uhamisho wa Waziri mmoja ambaye ni Profesa Makame Mnyaa Mbarawa kutoka Wizara ya Maji na Umwagiliaji na kwenda Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Kufuatia uteuzi huu, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue anawaarifu Mawaziri wote na Naibu Waziri walioteuliwa kuwa wataapishwa Jumatatu tarehe 28 Desemba, 2015 Saa tatu asubuhi, Ikulu Jijini Dar es salaam.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
24 Desemba, 2015
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment