Nkupamah media
Na Mwandishi Wetu
CHAMA cha muziki wa Injili
Tanzania (CHAMUITA) kimetoa wito kwa waamini kujitokeza kwa wingi kwenye
Tamasha la Krismasi linalotarajia kufanyika kesho kwenye ukumbi wa
Diamon Jubilee jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa
Chamuita, Addo Novemba tamasha hilo ni kubwa ambalo
waamini hawastahili
kulikosa kwa sababu ya umuhimu wa tamasha hilo.
Novemba alisema tamasha hilo
lina dhamira mbili ambazo ni sikukuu ya kuzaliwa kwa Masiha na pili ni
kurudisha shukrani kwa Mungu baada ya uchaguzi Mkuu uliofanyika kwa
amani, Oktoba 25 mwaka huu.
“Msama Promotions wanafanya kazi
kubwa katika muziki wa injili na kumtangaza Mungu, hivyo ni nafasi ya
waumini kujitokeza kumpa sapoti Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi, Alex
Msama ili kufanikisha matakwa ya jamii yenye uhitaji maalum,” alisema
Novemba.
Naye Katibu Mkuu wa Makanisa ya
Kipentoste Tanzania, Askofu David Mwasota alisema tamasha hilo ni muhimu
kwa sababu tumnasherehekea amani yetu.
Askofu Mwasota alisema wakazi wa
Dar es Salaam na mikoa ya karibu kujitokeza kwa wingi kwenye tamasha
hilo ambalo ni muhimu kwa Tanzania ijayo.
Askofu Mwasota alisema kusanyiko
la wote ni kusanyiko la Mungu hivyo waumini wajitokeze kwa wingi ili
kumrudishia Mungu shukrani baada ya kupita kwenye uchaguzi Mkuu
uliofanyika kwa amani na utulivu.
“Tuanatam,bua kila mtu ana imani yake lakini tunatoa wito wa kila mmoija kukusanyika ili kumfikishia Mungu shukrani,” alisema.
0 comments :
Post a Comment