Tume ya Taifa ya Uchaguzi imetoa
uamuzi wa mwisho kuhusu idadi ya Madiwani wa Viti Maalum katika
Halmashauri ya wilaya ya Kyerwa kuwa ni Madiwani wanne kutoka Chama Cha
Mapiduzi (CCM) na wanne kutokaChama Cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA).
Tume imefikia uamuzi huu kufuatia
malalamiko yaliyotolewa na CHADEMA, kwa nyakati tofauti
. Awali
ilibainika kuwa Matokeo ya Udiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya
Kyerwa yalikuwa na kasoro ambapo ilionyesha kuwa CCM walishinda kata 13
na CHADEMA walishinda kata 11 ambapo ukweli ni kuwa CCM walishinda kata
11 na CHADEMA walishinda kata 13.
Pili,CHADEMA iliwasilisha
malalamiko kuwa Tume imeibeba CCM kwa kuipa Madiwani 5 wa viti maalumu
na CHADEMA madiwani 4 wa viti maalum jambo ambalo lilisababishwa na
kasoro ya matokeo ya Uchaguzi wa Madiwani.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi baada
ya kupokea malalamiko hayo ilifuatilia kwa Msimamizi wa Uchaguzi jimbo
la Kyerwa ili kupata ufafanuzi kuhusu kasoro hizo za matokeo ya udiwani
ambapo Msimamizi wa uchaguzi aliwasilisha matokeo sahihi ambayo
yalionyesha kuwa CCM ilipata viti vya Kata 11 vya Udiwani na CHADEMA
viti vya Kata 13, hatua ambayo ililazimu kufanya upya mgawanyo wa viti
maalumu kwa kuzingatia kifungu cha 35(1) (c) cha Sheria ya Serikali za
Mitaa (Mamlaka za Wilaya) Sura ya 287 na baada ya marekebisho hayo Tume
ilimtaarifu Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Kyerwa kupitia barua yenye
kumb Na.AB.74/141/01 ya tarehe 08 Desemba,2015 kuhusu marekebisho ya
viti maalumu vya Udiwani wanawake na hivyo kufanya CCM kupata viti 4 na
CHADEMA viti 4 na kufanya idadi ya Madiwani wanawake wa Viti maalumu
kuwa 8 badala ya 9 vya awali.
Aidha, Tume ya Taifa ya Uchaguzi imetaja majina ya madiwani wa viti Maalum katika Halmashauri ya Kyerwa kama ifuatavyo:
Madiwani wa Viti Maalumu kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
- Restuta Kokuberwa Kafupa,
- Hyasinta Tibatekeleza Katia,
- Hassanat Muzeiyana Chamani, na
- Devotha Mkamungu Byashora.
Madiwani wa viti Maalum wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ni
- Devotha Nestory Ikambuza,
- Consolata Sebastian Kanyima,
- Joyleth Godwine Mutashaga na
- Theophila Kokwenda Theobard.
Marekebisho yaliyofanywa na Tume
ya Taifa ya Uchaguzi tarehe 08, Desemba, 2015 na kutumwa Halmashauri ya
Kyerwa yanapaswa kuzingatiwa katika hatua nyingine zinazofuata katika
Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
Imetolewa na
Jaji Mst DAMI.AN Z. LUBUVA
MWENYEKITI
TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI
0 comments :
Post a Comment