Mwenyekiti wa Umoja wa Rufaa ya
Wananchi (URUWA) John Shibuda akitoa pongezi kwa Serikali ya Awamu ya
Tano ya Rais Magufuli alipokuwa akiongea na Waandishi wa Habari leo
Jijini Dar es salaam.
Mwenyekiti wa Umoja wa Rufaa ya
Wananchi (URUWA) John Shibuda(katikati) akizungumza na waandishi wa
Habari (Hawapo pichani) wakimpongeza Rais wa awamu ya tano Dkt John
Pombe Magufuli kwa uongozi uliotukuka (Kulia) ni mjumbe wa umoja huo
Kaimu Katibu Mkuu – UDP Isaac Cheyo, wa pili kushoto Katibu Mkuu wake
Mwenyekiti Taifa – UPDP Fahami Nassoro Dovutwa na kushoto ni mjumbe wa
umoja huo Makamu Mwenyekiti- SAU Yusuf Salum Manyanga.
Mwenyekiti wa Umoja wa Rufaa ya
Wananchi (URUWA) John Shibuda(katikati) akisistiza jambo kwa waandishi
wa Habari wakati umoja huo walipokuwa wakitoa pongezi kwa Rais wa Awamu
ya Tano.
Picha Na Raymond Mushumbusi MAELEZO
…………………………………………………………………………………………..
Na Lilian Lundo MAELEZO
Uongozi unaounda mashirikiano ya umoja wa
vyama visivyo na Ruzuku ya Serikali ambavyo ni ADA-TADEA, UDP, UPDP na
SAU uitwao URUWA (Umoja wa Rufaa ya Wananchi) umeipongeza Serikali ya
Awamu ya Tano kwa uongozi uliojaa utukufu wa uzalendo.
Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa URUWA John Shibuda leo Jijini Dar es Salaam alipokuwa akiongeo na waandishi wa habari.
“Tunamuunga mkono Rais John Pombe Magufuli
kwa juhudi zake za utumishi aminifu na tiifu kwa ustawi na maendeleo ya
Jamii na Taifa, hongera sana kwa uongozi wako uliojaa utukufu wa
uzalendo na Neema ya kauli aminifu ya HAPA KAZI TU ambayo ipo kwa
maslahi ya Tanzania,” alisema Shibuda.
Umoja huo pia umepongeza
mshikamano wa uzalendo na uwajibikaji makini unaotekelezwa na Makamu wa
Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa.
Shibuda aliongeza kwa kusema kuwa wananchi
wa makundi yote yasiyotarajia kuingia katika kundi la uchumi wa kati
sasa wanamatumaini ya kufikia uchumi wa kati kutokana na kupata utumishi
sikivu kwa vilio vyao vya muda mrefu vya kupata maisha bora.
Aidha, uongozi wa umoja huo umesema kwamba
unaunga mkono juhudi zote zinazotekeleza Serikali ya Awamu ya Tano
katika kulisukuma mbele gurudumu la maendeleo ya Jamii na Taifa. Pia
wameitaka Serikali ya Awamu ya Tano kuendelea kutakatisha na kung’arisha
usafi wa mazingira ya uwajibikaji wa safari ya ukombozi ya ASP na TANU.
Umoja wa vyama visivyo na Ruzuku ya Serikali
URUWA umeundwa tarehe 18/12/2015 huku Mwenyekiti wa Umoja huo akiwa ni
John Shibuda ambaye ni Katibu Mkuu- ADA-TADEA, Katibu Mkuu akiwa ni
Fahami Nassoro Dovutwa ambaye ni Mwenyekiti Taifa – UPDP.
Wajumbe wa umoja huo ni Isaac Cheyo ambaye
Katibu Mkuu – UDP, Paul Kyara Mwenyekiti SAU na Yusufu Manyanga ni
Makamu Mwenyekiti – SAU.
0 comments :
Post a Comment