DAR ES SALAAM
Waziri wa Afya,Maendeleo ya
Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu ameagiza vituo vyote vya
serikali vya kutolea huduma za afya nchini, kwenye dirisha la
mapokezi,vyumba vya madaktari na sehemu ya
dawa zinaandikwa “mpishe mzee kwanza apate huduma”.
Agizo hili linakwenda sambaba na uwepo wa madirisha ya wazee katika vituo vyote vya serikali vya kutolea huduma za afya.
Mhe Ummy pia amehidi kupeleka Bungeni
Mswada wa Sheria ya Taifa ya Wazee ktk Bunge la mwezi Septemba ili
kuhakikisha haki na stahili za wazee nchini zinatekelezwa kikamilifu.
Wazee walieleza kero zao kubwa ni kupata matibabu, kutokuwa na kipato
cha uhakika na vitendo vya kudharauliwa na jamii.
0 comments :
Post a Comment