Rais Magufuli Asema Hataki Kusikia Malalamiko ya Wananchi juu ya Suala la Njaa......Ikitokea Akasikia, Mkuu wa Mkoa Atafukuzwa Kazi


Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh John Magufuli amesema kuanzaia sasa hataki kusikia malalamiko ya wananchi juu ya suala la njaa na ikitokea akasikia vilio hivyo vikiendelea mkuu wa mkoa husika atachukuliwa hatua
ikiwemo ya kufukuzwa kazi.
 
Mh. Magufuli ambaye yuko katika ziara ya kikazi mkoani Arusha ameyasema hayo alipokuwa njiani kutoka jijini Arusha kwenda wilaya Monduli kwa ajili ya kufunga mazoezi ya kijeshi ya kuonyesha uwezo wa medani 2016 yaliyofanyika katika Briged ya 303 iliyoko Monduli.

Aidha Mh rais Dr. Magufuli amesema ni jambo halikubali kuendelea kusikia malalamiko ya wananchi juu ya mambo yaliyoko ndani ya uwezo na yanayoweza kutatuliwa na wakuu wa mikoa na ameendelea kuwataka viongozi na watendaji wa serikaali kutimiza wajibu ukiwemo wa kuwatumikia wananchi.

Kuhusu malalamiko ya wananchi juu ya kero ya rushwa mh Rais amewataka wananchi hao kuwa wapole kwani kero itashughulikiwa na itapata ufumbuzi kwani zoezi la kutumbua majipu linaendelea na kwamba kinachofanyika sasa ni  kutumbua majipu yaliyoiva ambayo ni sehemu ndogo tu ya majipu yaliyopo.

Mh Rais kesho anatarajiwa kutoa kamisheni kwa askari wanafunzi katika chuo cha mafunzo ya kijeshi cha TMA monduli
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment