Mkuu wa Kituo cha Uhamiaji
mpakani Tarakea, wilayani Rombo Mkoa wa Kilimanjaro, John Kapembe
akimuonyesha Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja
Jenerali Projest Rwegasira (wapili kushoto aliyevaa kiraia) eneo la
Tanzania katika mpaka huo uliopakana na nchi ya Kenya. Rwegasira yupo
mkoani humo kwa ziara ya kikazi akitembelea vituo vya Uhamiaji vya
mipakani mkoani humo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Afisa Uhamiaji Mkoa (RIO) wa
Kilimanjaro, Naibu Kamishna Ambrose Mwanguku (kulia) akimkaribisha
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest
Rwegasira (wapili kulia) wakati alipowasili katika Jengo la Kituo cha
Pamoja cha huduma mpakani Holili, wilayani Rombo, Mkoa wa Kilimanjaro
kwa ajili ya ziara ya kikazi ya kutembelea mipaka ya Uhamiaji mkoani
humo Watatu kulia ni Kaimu Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Victoria
Lembeli.
Kaimu Kamishna Jenerali wa
Uhamiaji, Victoria Lembeli akimkaribisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo
ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (katikati meza kuu)
azungumze na Maafisa wa Idara ya mbalimbali za Serikali wanaotoa huduma
katika Kituo cha Pamoja cha Huduma Mipakani Holili wilayani Rombo, Mkoa
wa Kilimanjaro. Rwegasira aliwataka maafisa hao wafanye kazi kwa
ushirikiano ili kuiletea maendeleo nchi yao.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (katikati meza kuu)
akizungumza na Maafisa wa Idara ya mbalimbali za Serikali wanaotoa
huduma katika Kituo cha Pamoja cha Huduma Mipakani cha Holili, wilayani
Rombo, Mkoa wa Kilimanjaro. Meja Jenerali Rwegasira katika hotuba yake
aliwataka maafisa hao wafanye kazi kwa ushirikiano ili kuiletea
maendeleo nchi yao.
Kaimu Mkuu wa Kituo cha Uhamiaji
mpakani Holili, Edwin Mwasota akimuonyesha Katibu Mkuu wa Wizara ya
Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (watatu kulia)
moja ya ofisi zilizopo katika Jengo la Kituo cha Pamoja cha Huduma
Mipakani cha Holili, wilayani Rombo, Mkoa wa Kilimanjaro. Wapili kushoto
ni Kaimu Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Victoria Lembeli. Meja Jenerali
Rwegasira alifanya ziara ya kikazi kwa kutembelea vituo vya Uhamiaji
vya mipakani mkoani Kilimanjaro.
Afisa Uhamiaji Mkoa (RIO) wa
Kilimanjaro, Naibu Kamishna Ambrose Mwanguku (kushoto) akimuonyesha
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest
Rwegasira (wapili kushoto) mpaka Tanzania pamoja na Jengo la Uhamiaji la
nchini Kenya (Taveta) wakati walipokuwa juu ya ghorofa ya Jengo la
Kituo cha Pamoja cha Huduma Mipakani Holili, wilayani Rombo, Mkoa wa
Kilimanjaro.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (wapili kushoto aliyevaa
kiraia) akiondoka katika Jengo la Kituo cha Pamoja cha Huduma Mipakani
Holili, wilayani Rombo, Mkoa wa Kilimanjaro mara baada ya kumaliza ziara
yake ya kulitembelea jengo hilo na kuzungumza na maafisa mbalimbali wa
serikali wanaotoa huduma za mpakani mkoani humo. Kushoto ni Afisa
Uhamiaji Mkoa (RIO) wa Kilimanjaro, Naibu Kamishna Ambrose Mwanguku na
Kulia ni Afisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika mpakani
Holili, Aden Mwakalobo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.


0 comments :
Post a Comment