TANZANIA KUANZA NA SHELISHELI U-17

Nkupamah media

Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) limetoa ratiba ya kuwania kufuzu kwa Fainali za Mataifa Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 (U-17) zitakazofanyika nchini Madagascar mwakani kwa timu ya Taifa ya Tanzania (Serengeti Boys) kuanza na Shelisheli.

Katika ratiba hiyo iliyotolewa makao makuu ya CAF, Cairo Misri na nakala yake kutumwa kwa TFF, Tanzania imepangwa kucheza mchezo wa kwanza dhidi ya Shelisheli kati ya Juni 24,25,26 nchini na marudaino kuchezwa Julai 01,02,03 nchini Shelisheli.
Mshindi kati ya mchezo huo namba 15 na16 atacheza dhdi ya timu ya Taifa ya  Afrika Kusini katika hatua inayofuata ya 16 bora, na kisha baadae kupata timu 8 zitakazofuzu kwa fainali hizo zitakazofanyika nchini Madagascar mwakani.
Fainali za Kombe la Dunia (FIFA U17) kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 zitafanyika mwezi Septemba waka 2017 nchini India.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment