Nkupamah media:
Kiti cha
urais wa Shirikisho la Soka duniani (FIFA) kimepata rais mpya baada ya
miaka 18 kushikiliwa na Sepp Blatter baada ya kufanyika uchaguzi usiku
wa Ijumaa na Gianni Infantino kufanikiwa kushinda nafasi hiyo.
Infantino
amefanikiwa kushinda nafasi hiyo ya juu FIFA baada ya kuwashinda
wapinzani wake ambapo amepata kura 115, Sheikh Salam 88, Prince Ali
al-Hussein 4 na Jerome Champagne akikosa kura kabisa.
Baada ya
matokeo hayo kutangazwa Infantino ameonekana mtu mwenye furaha kwa
kupata ushindi huo na kusema kuwa “Wapendwa, siwezi kusema jinsi
ninavyojisikia kwa wakati huu” alisema na kuongeza.
“Niliwaambia
ninakwenda safarini, safari ya kipekee, safari ambayo itanifanya
nikutane na watu tofautitofauti wengi wao wakiwa wapenda soka, wanaoishi
katika soka, wanaopumua katika soka kila siku na watu wengi ambao
wanastahili heshima hii kutoka FIFA”(P.T)


0 comments :
Post a Comment