Ligi
ya Mabingwa ya barani Ulaya iliendelea jana kwa michezo ya kwanza ya
hatua ya 16 bora ambapo michezo miwili ilichezwa. Benfica ya Ureno
iliikaribisha Zenit St. Petersburg na mchezo wa pili ukiwa ni Paris
Saint-German iliyokuwa mwenyeji wa Chelsea ya Uingereza.
Mchezo
wa PSG na Chelsea ulimalizika kwa PSG kuibuka na ushindi wa goli mbili
kwa moja, magoli yakifungwa na Zlatan Ibrahimovic dakika ya 19 na Edson
Cavani dakika ya 78 na goli la Chelsea likifungwa na John Obi Mikel.
Mchezo
mwingine ulimalizika kwa wenyeji Benfica kuibuka na ushindi wa goli
moja kwa bila, goli likifungwa na Jonas Oliveira katika dakika ya 90+1.


0 comments :
Post a Comment