Elisabet alipokuwa mdogo wa miaka miwili na nusu alichukuliwa na watu wawili raia wa Sweden ambao walimchukua kwenda kuishi nae kutoka katika kituo kilichokuwa kikimlea.
Alieleza kuwa wakati akiwa Sweden alitaka kwenda kumtafuta mama yake lakini walezi wake walimtaka aendelee na maisha yake bila kumtafuta lakini alikwenda mwaka 1998 kumtafuta lakini ilikuwa sio rahisi kumpata na ndipo mwaka 2014 alipoamua kuwasiliana na Shirika linalopinga vitendo vya wizi wa watoto (ACT).
Aliongeza kuwa Agosti, 8 mwaka jana alipokea taarifa za kupatikana kwa mama yake kutoka ACT na kumtumia baadhi ya picha za mama yake.
“Siwezi kuelezea hisia zangu, ni mtu ambaye nilikuwa naye mbali kwa maisha yangu yote alafu namuona kwenye picha, ulikuwa kama muujiza, ni muujiza mkubwa,” alisema Elisabet.
Chanzo: BBC