Bomu laua watu 50 Iraq

  • Nkupamah media:
Image copyrightAP
Image captionShambulizi la bomu laua watu 50 Iraq
Takriban watu 50 wameuawa katika mji wa Hillah Iraq baada ya mlipuaji wa kujitolea mhanga kulipua lori lililokuwa limejazwa vilipuzi.
Lori hilo la kubeba mafuta lilisogezwa karibu kabisa na kituo cha kupekulia magari nje ya mji mkuu wa Baghdad kabla ya kujilipua.
39 ya wale waliouawa walikuwa ni raia huku waliosalia wakiwa ni polisi.
Image copyrightGetty
Image caption39 ya wale waliouawa walikuwa ni raia huku waliosalia wakiwa ni polisi.
Shambulizi hilo lilitokea mwendo wa saa 9 asubuhi saa za mashariki ya kati.
Watu wengi zaidi walijeruhiwa.
Wakuu wanasema lori lilokuwa na mabomu, liliripuka, na kusababisha vifo, kati ya magari mengi yaliyokuwa yakisubiri kupekuliwa.
Image captionMji wa Hill uko kilomita mia moja kusini mwa Baghdad.
Mji wa Hill uko kilomita mia moja kusini mwa Baghdad.
Kundi la wapiganaji la Islamic State limedai kutekeleza shambulizi hilo kupitia mtandao wake wa Amaq.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment