Dar Swim club yawapongeza waogeaji wake kwa kufanya vyema mashindano ya Taifa

Nkupamah media:
wao1
Waogeleaji wa klabu ya Dar Swim wakipasha viungo moto kabla ya kuingia mashindanoni
wao2
Waogeleaji wakipasha viungo kwa staili ya backstroke
wao3
Waogeleaji wakipasha jinsi ya kupiga mbizi au ku-dive
………………………………………………………………………………………………………………………..
Na Mwandishi wetu
Klabu maarufu ya kuogelea jijini, Dar Swim Club imewapongeza waogeleaji wake kwa kufanya vyema katika mashindano ya taifa ya kuogelea yaliyomalizika hivi karibuni katika bwawa la Hopac.
Akizungumza jijini jana, Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Inviolata Itatiro alisema kuwa waogeaji wake wameweza kuboresha muda wa kuogelea na kuiwezesha klabu hiyo kutwaa nafasi ya kwanza kwa upande wa wanawake kwa kukusanya jumla ya pointi 1,964.50.
Inviolata alisema kuwa kwa upande wa wanaume, walikusanya jumla ya pointi 1,086.50 na kushika nafasi ya pili. Alisema kuwa wamefarijika na matokeo hayo kutokana na wao kuwakilishwa na waogeleaji chipukizi katika mashindano hayo.
“Hii ni faraja kwetu, tumeweka mikakati ya kukuza mchezo wa kuogelea kwa miaka 10, tunawaogeaji wadogo sana lakini wana vipaji vya hali ya juu, lakini kutokana na mfunzo mazuri ya makocha wetu, wameweza kuwashinda waogeleaji wenye umri mkubwa, kwa kweli wanastahili pongezi,”
“Wakati tunaanza, hatukutegemea kufikia hatua hii, tuliweza kutwaa medali 94 katika mashindano ya kuogelea ya Taliss na kushika nafasi ya kwanza na kuwa klabu bora, natoa wito kwa wazazi ambao wanataka watoto wao kujua kuogelea na kushindana katika mashindano ya ndani na kimataifa, kujiunga na klabu yetu,” alisema Inviolata.
Alisema kuwa mafanikio ya klabu yao yametokana na ushirikiano wao na wazazi na wadhamini mbalimbali ambao wamekuwa nguzo kubwa ya kufanikisha mambo kadhaa ya maendeleo ya mchezo wa kuogelea.
“Tuliweza kufanya semina kwa makocha na waogeleaji wetu chini ya mkufunzi wa kimataifa na muogeleaji nyota wa zamani wa Olimpiki, Penny Heyns wa Afrika Kusini. “Mafunzo yalikuwa ya kisasa na sasa tunajivunia matunda yake, nawashukuru makocha kwa kufanya kazi kubwa,” alisema.
Alisema kuwa makocha wao, Michael Livingstone, Ferick Kalengela, Radhia Gereza, Kanisi Mabena, Adam Kitururu, Simon Ngoya na Salum Mapunda wamekuwa nguzo kubwa ya kufikia malengo yao.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment