Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda aanza kazi rasmi..atoa masaa 24 kwa wakuu wa Idara


1 (1)Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alipowasilia ofisini kwake jijini Dar es Salaam mapema leo Machi 20.2016 kuanza kazi rasmi ya Ukuu wa Mkoa huo.


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ameanza kazi rasmi leo Machi 16.2016 majira ya mchana ambapo alifanya mazungumzo na wakuu wa idara na Vitengo mbalimbali na kutoa maagizo mazito ambapo alitoa masaa 24 kwa wakuu hao  kumpa taarifa zilizopo katika maeneo yao husika zenye kuelezea changamoto mbalimbali ili kuona wananchi wanakabiliwa na changamoto zipi na namna atakavyoweza kuzitatua.
Makonda aliyasema hayo wakati akizungumza na wakuu hao wa idara na vitengo katika hafla fupi ya kukaribishwa kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ambapo mbali ya wakuu hao wa idara na vitengo pia ilihudhuriwa na Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na Makatibu Tawala wa wilaya zote za mkoa wa Dar es Salaam. 
IMG_2056Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (katikati), akizungumza na wakuu wa idara mbalimbali katika ofisi yakea mapema leona kuwapa maagizo mbalimbali ndani ya masaa 24 wawe wamempatia zenye changamoto za kushughulikia.
IMG_2052 Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema, akimkabidhi kadi ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment