Baada
ya kuchelewa mazoezini na sababu yake kuwa ni amepuuzia kengele,
uongozi wa klabu yake ya Wolfsburg ulimpa adhabu ya kulipa Pauni 39 kwa
kila dakika aliyochelewa ambapo kwa dakika 45 ikawa ni Pauni 1,770 na
pia akaambiwa afanye mazoezi peke yake.
Akizungumza na gazeti la Ujerumani la Bild, Bendtner alisema “Nilipitiwa kulala, nilipuuzia kengele, ni kosa langu”
Hilo
sio kosa la kwanza la Bendtner kulifanya tangu alipowasili katika klabu
hiyo kwani hata mwezi uliopita alikwenda mazoezini akitumia gari aina
ya Mercedes S-Class licha ya kufahamu kuwa hawaruhusiwi kwenda mazoezini
na gari za kampuni nyingine kutokana na klabu hiyo kuwa na mkataba na
kampuni nyingine ya magari ya Volkswagen.


0 comments :
Post a Comment