Mwanafunzi Abakwa na Kuuawa kwa Kunyongwa

Nkupamah media:


Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Mnero iliyopo Tarafa ya Ruponda mkoani Lindi, ameuawa kwa kunyongwa baada ya kubakwa na wanaume wasiofahamika kisha mwili wake kutelekezwa kichakani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, Renatha Mzinga alisema jana kuwa mwanafunzi huyo alikuwa na tabia ya kuruka ukuta usiku na kwenda nje ya shule kufuata wanaume.

Kamanda Mzinga alisema mwanafunzi huyo alipofika kwenye kichaka hicho kilichopo karibu na eneo la Kanisa Katoliki alibakwa na wanaume hao kisha kumuua kwa kumnyonga.

Alisema wanamshikilia mwendesha bodaboda, mkazi wa Kijiji cha Mnero ngongo kwa mahojiano zaidi kuhusiana na tukio hilo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment