Chama cha Watoa Huduma za Mitandao ya Intaneti nchini kupitia mradi wa Tanzania Internet Exchange (TIX) imezindua mfumo mpya wa huduma ya intaneti ya kampuni ya Akamai ambao utawawezesha watumiaji wa intaneti nchini kupata huduma kwa uharaka zaidi.
Akizungumzia huduma hiyo, Meneja Mradi wa TIX, Frank Habicht alisema kupita huduma hiyo watumaji wa intaneti nchini wataweza kuperuzi katika mtandao kwa spidi zaidi kutokana na kasi ya mawasiliano ya intaneti inayopatikana katika mfumo huo wa Akamai.
Alisema wameamua kutumia huduma kutoka Akamai kutokana na ubora wa huduma zinazopatikana katika kampuni hiyo na pia wana mitambo ya kutolea huduma katika maeneo mengi duniani.
“Kupitia huduma hii wateja watatumia intaneti kwa gharama nafuu na hivyo itaweza kuboresha upatikanaji wa intaneti kwa watumiaji wa Tanzania na ni nzuri sababu inauwezo wa kuunganisha watu wengi kwa wakati mmoja na wakapata huduma iliyo nzuri,” alisema Habicht.
Kwa upande wa mgeni rasmi Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amewashukuru TISPA kwa kutimiza ahadi waliyoitoa mwaka jana ya kuongeza jitihada ili kupata huduma nyingi zaidi za mifumo ya intaneti ili kurahisisha gharama za intaneti nchini.
Alisema serikali imekuwa ikifanya juhudi mbalimbali ili kuboresha sekta hiyo na kama kunakuwepo na watu wanaowapa sapoti ili kuboresha huduma ya intaneti ni jambo la kupendeza.
“Nimefurahi kuwepo hapa mwaka jana nilikuja na mwaka huu nimekuja tena kwa ajili ya uzinduzi wa huduma ya intaneti ambayo itarahisisha huduma ya intaneti, hongereni sana,” alisema Prof. Mbarawa.
Aidha waziri amewataka TISPA kufanya jitihada zaidi ili ikiwezekana mwakani waweze kuzindua mfumo mwingine wa huduma kutoka Limelight na Amazon.
Nae Mwenyekiti wa TISPA, Vinay Choudary alisema wamekuwa wakifanya jitihada mbalimbali ili kuboresha huduma ya intaneti nchini na wataendelea kuwa mstari wa mbele katika kuanzisha huduma bora za intaneti na bora,
DSC_1369Mwenyekiti wa TISPA, Vinay Choudary akizungumzia kazi wanazofanya kwa sasa na mipango ambayo wanaifanyia kazi.
DSC_1388Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akitoa neno kwa niaba ya serikali.
DSC_1394
DSC_1409Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akifanya uzinduzi wa mfumo huo wa huduma ya intaneti, Kulia ni Mwenyekiti wa TISPA, Vinay Choudary.
DSC_1410
DSC_1420Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akimwambia jambo Mwenyekiti wa TISPA, Vinay Choudary baada ya zoezi la uzinduzi kukamilika.
DSC_1422Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akiagana na Mwenyekiti wa TISPA, Vinay Choudary.
DSC_1423Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa akiagana na Meneja Mradi wa TIX, Frank Habicht.
DSC_1351Meneja Mradi wa TIX, Frank Habicht akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mradi huo.
DSC_1426Mitambo ambayo itatumika kutoa huduma hiyo.