Meneja utetezi wa Oxfam Tanzania, Eluka Kibona amesema uelewa wa wanawake katika kumiliki
ardhi na kufuatilia haki zao za ardhi unaongezeka siku hadi siku nchini
na kuondoa ile dhana kwamba wanawake wako nyuma katika shughuli za
maendeleo.
Bi
Eluka ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na Blogs za Mikoa kuhusu
namna taasisi binafsi zinavyotetea harakati za wanawake katika kumiliki
ardhi hapa nchini na kujiendeleza kiuchumi ambapo amesema kwa
kulinganisha miaka 10 iliyopita na sasa, wanawake kwa sasa wamekuwa na
muamko zaidi wa kupambana na changamoto za umiliki wa ardhi wanazokutana
nazo.
”Sisi tunaunga
mkono harakati na jitihada za kuleta usawa kati ya wanaume na wanawake
mjini na vijijini na hii ni baada ya kutambua kuwa matatizo ya umiliki
wa ardhi kwa wanawake wa mjini na vijijini yako sawa kutokana na
mfumo ulivyo katika jamii.”Ameeleza Bi Eluka.
mfumo ulivyo katika jamii.”Ameeleza Bi Eluka.
Mmoja wa wanawake (Kulia) akipokea hati yake ya kumiliki ardhi kutoka kwa Mkurugenzi Mkazi wa Oxfam Tanzania Jane Foster katika kijiji cha Gongoni wilayani Kilosa.
”Kuna
madai ya ardhi ambayo wanawake wanakumbana nayo katika jamii kwa
kudhulumiwa na wengine kwa kunyimwa haki zao za msingi hivyo
tunawasaidia katika kuwawezesha kutambua namna ya kupigania haki
zao.”Amesisitiza Bi Eluka.
Kuhusu siku ya wanawake duniani ambayo huazimishwa kila Machi 8 kila mwaka,
Bi Eluka amesema Oxfam Tanzania imejipanga kufanya maadhimisho katika
mkoa wa Mtwara ili kuunga mkono jitihada za wanawake katika kujikwamua
na mifumo kandamizi hapa nchini na kujiendeleza kiuchumi.
Mmoja wa wanawake akiwa katika kilimo
Kwa mujibu wa Bi Eluka, Oxfam imewezesha wanawake wengi kuweza kupata haki zao katika mikoa mbalimbali nchini na baadhi ya mikoa hiyo ni Shinyanga, Arusha, Tanga Morogoro/
Kwa mujibu wa Bi Eluka, Oxfam imewezesha wanawake wengi kuweza kupata haki zao katika mikoa mbalimbali nchini na baadhi ya mikoa hiyo ni Shinyanga, Arusha, Tanga Morogoro/
Aidha kwa mujibu wa sheria ya ardhi inatamka bayana kuwa mwanamke ana haki sawa na mwanaume katika kupata, kumiliki, kutumia na kugawa ardhi. (Kifungu 3(2) cha sheria ya ardhi na sheria ya ardhi ya vijiji za 1999).
Hata hivyo
ni muhimu kila mmiliki wa ardhi awe na hati/ cheti halisi
cha hakimiliki kuthibithisha haki yake ya kumiliki ardhi kisheria.
0 comments :
Post a Comment