Aliyemtukana Mtume Kuadhibiwa Kifo Nchini Mauritania


Mahakama ya Rufaa ya Mauritania imepasisha hukumu ya kifo dhidi ya mwandishi aliyemvunjia heshima Mtume Muhammad (saw).

Shirika la Habari la Kimataifa la Qur'ani (IQNA) limeripoti kuwa, Mahakama ya Rufaa ya mji wa Nawadibo huko kaskazini magharibi mwa Mauritania imepasisha hukumu ya kifo dhidi ya mwandishi Muhammad Sheikh Ould Amkhtir wa nchi hiyo kwa sababu ya kuandika makala iliyomvunjia heshima na kumtusi Mtume wa Mwenyezi Mungu, Muhammad (saw) hapo mwaka 2014.

Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mauritania ambaye aliomba kutolewe hukumu ya kifo dhidi ya mwandishi huyo amesema kuwa kunyongwa kwake kutakuwa somo kwa wale wote wanaothubutu kumvunjia heshima Mtume wa Mwenyezi Mungu.

Kuchapishwa kwa makala ya mandishi Muhammad Sheikh Ould Amkhtir hapo mwaka 2014 kulisababisha maandamano makubwa kote Mauritania ambayo hayakutulia ila baada ya kutolewa hukumu ya kifo dhidi ya mwandishi huyo.
Share on Google Plus

About Mng'atuzi blog

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment