Picha
za matukio ya Heart Marathon iliyofanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu
cha Dar es Salaam ambapo ilihusisha mbio za urefu wa 21Km, 10Km, 5Km,
mita 700 kwa ajili ya watoto, Baiskeli Kilomita 21 na Baiskeli walemavu.
Washiriki wa mbio za Heart Marathon kwa waendesha Baiskeli wakiwa katika mashindano hayo jana jijini Dar es Salaam.
Watoto wakiwa katika mashindano ya Heart Marathon mbio za urefu Mita 700 jana jijini Dar es Salaam.
Wanariadha washiriki wa Heart Marathon wakichuana katika mbio za urefu wa kilomita 21 jana jijini Dar es Salaam.
Kaimu
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Alex Nkenyenge akimvalisha Medali mshindi wa kwanza kwa
wanaume mbio za Kilomita 21 Bw. Dickson Marwa wakati wa ufungaji wa
mbio za Heart Marathon zilizofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Kaimu
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Alex Nkenyenge akimvalisha Medali mshindi wa kwanza kwa
wanawake mbio za Kilomita 21 Bibi. Failuna Abdi wakati wa ufungaji wa
mbio za Heart Marathon zilizofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Kaimu
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Alex Nkenyenge akikabidhi Tuzo kwa mdhamini mkuu wa
mbio za Heart Marathon, Taasisi ya Tindwa Medical and Health Services
wakati wa ufungaji wa mbio za hizo jana jijini Dar es Salaam. Mbio hizo
zilikuwa na kauli mbiu ya “Kuwa huru katika magonjwa yasiyo ya
kuambukiza”.
Kaimu
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Alex Nkenyenge akizungumza na wadau wa riadha wakati wa
ufungaji wa mbio za Heart Half Marathon zilizofanyika jana katika
viwanja vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kulia ni Rais wa Kongamano la
Afya Tanzania na Mratibu wa mbio hizo Dkt. Omary Chillo.
Mwenyekiti
wa Kamati ya maandalizi ya Heart Marathon Dkt. Chakao Khalfan
akizungumza na waandishi wa Habarai mara baada ya kumalizika kwa mbio
hizo jana jijini Dar es Salaam. Heart Marathon hii imejumuisha mbio za
urefu wa 21Km, 10Km, 5Km, mita 700 kwa ajili ya watoto, Baiskeli
Kilomita 21 na Baiskeli walemavu.(Picha na: Frank Shija, WHUSM).


0 comments :
Post a Comment