Watumishi Hewa 14 Kufikishwa Mahakamani



Halmashauri ya Wilaya ya Muheza mkoani Tanga inatarajia kuwafikisha mahakamani watumishi hewa  14

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Adrian Jungu aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake juzi kuhusiana na hatua iliyochukua baada ya kubainika kuwa halmashauri yake ina watumishi hao hewa.

Jungu alisema mwanasheria wa halmashauri hiyo anaandaa utaratibu wa kuwafikisha mahakamani watumishi hao ambao walikuwa wakipokea mishahara wakati hawapo katika vituo vyao vya kazi.

Alisema watumishi hao ni walimu na hakukuwa na taarifa zozote za sababu za kutokuwapo kwao katika vituo vyao vya kazi.

“Nitawachukulia pia hatua kali wakuu wa idara ambao watabainika walikuwa na watumishi ambao hawakuwa katika vituo vyao vya kazi bila taarifa,” alisema.

Alisema adhabu hiyo itawakumba pia walimu wakuu wa shule kwa kosa la kushindwa kuripoti utoro wa walimu hao kwenye idara husika.

Mkurugenzi huyo aliahidi kuendeleza kazi ya uhakiki watumishi kila baada ya miezi sita ili kukomesha tabia hiyo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment