Michezo
ya hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya imeendelea usiku wa
Jumatano kwa michezo miwili, Wolfsburg wakiwa wenyeji wa Real Madrid na
PSG ikiwakaribisha Manchester City.
Matokeo
ya michezo hiyo Wolfsburg iliibuka na ushindi wa goli mbili kwa bila
dhidi ya Real Madrid, magoli yakifungwa na Ricardo Rodriguez dk. 18 na
Maximilian Arnold dakika ya 25.
Mchezo
mwingine PSG ilitoka sare ya magoli mawili kwa mawili, magoli PSG
yakifungwa na Zlatan Ibrahimovic dk. 49 na Adrien Rabiot na dakika ya 59
na magoli ya Manchester City yakifungwa na Kevin De Bruyne dk. 38 na
Fernandinho dk. 72.


0 comments :
Post a Comment