Mshambuliaji
wa Leicester City, Jamie Vardy ametajwa na Chama cha Waandishi wa
Habari cha Uingereza (FWA) kuwa mchezaji bora wa msimu wa 2015/2016.
Akimtaja
Jamie Vardy kuwa mshindi wa tuzo hiyo, Mwenyekiri wa FWA, Andy Dunn
amesema kumekuwepo na wachezaji wengi ambao wamekuwa bora kwa msimu huu
lakini Jamie Vardy amekuwa bora zaidi.
“Ni
uamuzi wa waliohusika kuchagua, kulikuwa na wachezaji wengi wa
Leicester ambao walitajwa na wenzetu lakini Jamie Vardy kaacha historia,
ni kweli ametajwa na waandishi wengi,” alisema Dunn.


0 comments :
Post a Comment