Washika bunduki wa London, Arsenal wanajipanga kupeleka ofa kwa mabingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza 2015/2016, Leicester City ili kupata saini ya mshambuliaji wa klabu hiyo, Jamie Vardy.
Mtandao wa TheGuardian wa nchini Uingereza umeeleza kuwa Arsenal inajipanga kupeleka ofa ya Pauni Milioni 22 baada ya kuwepo kwa kifungu ambacho kinamruhusu Vardy kujiunga na klabu nyingine ambayo atakuwa amekubaliana nayo kwa ajili wa mustakabali wa maisha yake ya baadae kisoka.
Aidha inasemekana kuwa Leicester City inahitaji kitita cha Pauni Milioni 30 ili kumwachia Vardy ambaye mwezi Februari mwaka huu aliongeza mkataba kuendelea kuichezea klabu hiyo.
Blogger Comment
Facebook Comment