Wananchi wa Uingereza bado wapo katika majonzi ya timu yao ya taifa kuondolewa katika mashindano ya Uefa Euro 2016 na Iceland kwa kichapo cha goli 2-1 katika hatua ya 16, hali hiyo ni tofauti kwa nahodha wa zamani wa timu hiyo, John Terry.
Kupitia akaunti yake ya Twitter, Terry ameweka picha akiwa na mke wake katika moja ya fukwe zilizopo Uingereza na kuweka picha zingine akiwa ‘gym’ akifanya mazoezi kujiandaa na msimu mpya wa 2016/2017.
Terry ambye kwasasa ana miaka 35 anataraji kuwepo katika kikosi cha Chelsea cha msimu ujao baada ya kuongezewa mkataba wa mwaka mmoja na kocha mpya wa Chelsea, Antonie Conte.
John Terry
John Terry
John Terry na mke wake