Majina
ambayo mashabiki wa Manchester United wamekuwa wakimuita Zlatan
Ibrahimovic tangu alipowasili klabuni hapo yanaonekana kuanza kumponza
baada ya mkongwe wa klabu hiyo, Eric Cantona kutoa maneno ambayo
yanaonekana kumtahadharisha Ibra kuhusu heshima anayopewa na mashabiki.
Mashabiki
wa Man United wamekuwa wakimuita Ibrahimovic, mfalme lakini Cantona
amemwambia kuwa kumeshawahi kuwa na mfalme mmoja tu katika klabu hiyo
na kama akitaka kupata nafasi basi atakuwa mtoto wa mfalme “Prince”.
“Nina
ujumbe binafsi kwa Zlatan, umechagua kwenda Man United, ni uamuzi
sahihi ambao umeufanya,” Cantona alisema wakati akifanya mahojiano na
Eurosport na kuongeza.
“Jambo
moja ni kuwa kuna mfalme mmoja Manchester. Unaweza kuwa mtoto wa mfalme
kama ukihitaji na jezi namba 7 ni yako kama ukihitaji. Hii ndiyo zawadi
yangu ya ukaribisho kwako. Mfalme ameshaondoka, nakutakia mafanikio
mema mtoto wa mfalme”


Blogger Comment
Facebook Comment