Mbeya City kucheza mchezo maalum na Mtibwa Sugar Julai 30



SIKU  kadhaa baada ya kuanza kwa kambi ya mazoezi kwa ajili ya matayarisho ya msimu mpya tayari  imethibitishwa  kuwa kikosi cha Mbeya City fc kitasafiri mpaka mkoani Morogoro kwa ajili ya mchezo wa kujipima nguvu dhidi ya wenyeji Mtibwa Sugar kwenye uwanja wa Jamhuri   julai 30.
Kwa mujibu wa kiongozi wa Kanisa la Faith Baptist, Mch  Jerry Wyatt ambaye ndiye mwandaaji na msimamizi mkuu wa mchezo huo,maandalizi yote ya mechi hiyo ya kirafiki itakayoambatana na tamasha kubwa la mahubiri ya neno la Mungu tayari yamekamilika ikiwa ni pamoja na timu zote kuthibitisha kuhudhuria.
“Maandalizi yote yamekamilika, timu zote zimethibitisha kushiriki katika mchezo huo ambao  utaambana na mahubiri ya neno la Mungu kwenye uwanja wa Jamhuri, naomba watu wajitokeze kwa wingi kuja kushuhudia mchezo mzuri wa kirafiki kutoka kwa timu hizi mbili pia kupata mahubiri mazuri ya neno la Mungu sambamba na matukio mengine mengi” alisema.
Akiendelea  zaidi Mch Jerry  alisema kuwa kwenye tamasha hilo la neno la Mungu na mchezo wa kirafiki wa soka hakutakuwa na kiingilio chochote kwa watakaofika kwenye uwanja wa Jamhuri na kwa wale watakaopata nafasi wanakaribishwa kuhudhuria ibada kwenye kanisa la Faith Baptist lililopo Kola B siku jumapili ya julai 31.
“Hakutakuwa na kiingilio, pia wale watakaopata nafasi nawakaribisha  kuhudhuria ibada kwenye kanisa letu  siku ya Jumapili siku ambayo  pia  tutatoa zawadi mbalimbali kwa timu za soka zaidi ya 40 za mjini hapa (Morogoro) kwa maana hiyo litakuwa jambo jema watu wote wakihudhuria”
Hii ni mara ya pili kwa Mtibwa na City kucheza mchezo wa kirafiki ulioandaliwa na Kanisa  hilo  awali ikiwa ni msimu uliopia ambapo timu hiyo kutoka Manungu iliibuka na ushindai wa bao 1-0 lililofungwa kipindi cha pili na Mohamed  Ibrahim
City  inatarajia  kuondoka  Mbeya  Julai  28 tayari  kwa mchezo huo  uliopangwa kupigwa  siku jumamosi ya mwisho wa mwezi huo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment