Dereva Taxi Jela Maisha Kwa Kulawiti Mtoto Ndani ya Gari



Mahakama ya Wilaya ya Ilala, imemhukumu kifungo cha maisha jela, dereva taksi Ally Mzako (29) baada ya kupatikana na hatia ya kumlawiti mtoto wa miaka mitano.

Mzako ambaye ni mkazi wa Kinondoni, anadaiwa kumbaka mtoto huyo ndani ya gari, wakati mama wa mtoto huyo alipomuacha katika gari hiyo na kwenda duka la kubadilishia fedha za kigeni.

Hakimu mkazi, Flora Haule amesema Mahakama imeridhishwa na ushahidi wa mashahidi sita wa  upande wa mashtaka dhidi ya mshtakiwa.

Mzako alifanya kosa hilo, Julai 19, 2014, eneo la Clock Tower, mtaa wa Samora.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment