Serikali
imepanga kuendesha zoezi maalumu la usajili na utoaji wa utambulisho na
vitambulisho vya Taifa kwa Watumishi wa Umma nchi nzima litakalodumu
kwa muda wa wiki mbili kuanzia Oktoba 3, 2016.
Watumishi
watakaosajiliwa ni waliopo katika Wizara, Idara za serikali
zinazojitegemea, Tawala za Mikoa, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Wakala
za Serikali na Taaaisi, Mashirika ya Umma.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Angellah Kairuki
wakati akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam
amesema lengo la zoezi hilo la usajiri ni kuondoa vyanzo vya watumishi
hewa vinavyotokana na utambulisho danganyifu.
“Serikali
inaendelea na zoezi la kuandaa utaratibu mmoja wa kukusanya, kutunza,
kutumia na kuhifadhi taarifa muhimu ili kuwa na chanzo kimoja sahihi.
Hatua hii itapunguza gharama za uendeshaji, kuongeza tija, ufanisi na
uwazi serikalini, ” amesema na kuongeza.
“Lengo
ni kuunganisha mifumo ya utambuzi wa watu na mifumo mbalimbali ikiwemo
usimamizi wa rasilimali watu na mishahara katika utumishi wa umma, pia
utasaidia kuondoa vyanzo vya watumishi hewa vinavyotokana na utambulisho
danganyifu.”
Kairuki
amesema usajili huo utaambata na uhakiki wa vyeti vya elimu, vya
kuzaliwa, hati ya kusafiria, kitambulisho cha kupigia kura na karatasi
za malipo ya mishahara ya watumishi hao.
Aidha, amesema watumishi watakaokaidi agizo hilo watachukuliwa hatua za kisheria kwa mujibu wa kanuni za utumishi wa umma.
“Data
zilizopo ni chafu, wakati mwingine ukifuatilia taarifa ya mtumishi
unakuta taarifa ya cheti cha kuzaliwa au elimu hakuna. Usajili huu
utavumbua mengi na wale wasio na sifa watajifukuzisha kazi wenyewe, ”
amesema.
Kairuki
amezitaka ofisi na taasisi zote za serikali kuandaa ratiba
itakayowezesha watumishi kufanya usajili pamoja na kutoa ushirikiano wa
kutosha ili kufanikisha zoezi hilo.
Na Regina Mkonde


0 comments :
Post a Comment