Siku kadhaa baada ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi kutoa maoni yake juu ya kile kinachoendelea katika Chama cha Wananchi (CUF) na baada ya hapo wanasiasa kuwa wakitumia jina lake kwa kupinga na wengine kukubali maoni yake, Jaji Mutungi ametoa taarifa kuhusu hilo.
Katika taarifa ambayo imetolewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Ofisi ya Msajili, Monica Laurent amesema kuwa kuna watu wamekuwa wakitumia jina la ofisi ya msajili kwa kuzungumza na vyombo vya habari na kwamba waache tabia hiyo.
press-release-04-oktoba-2016-page-001