Jeshi la Polisi kuanza msako wa kuwatafuta waliovunja viti vya Uwanja wa Taifa



Kamishna wa Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamanda Simon Sirro leo amesema jeshi lake linawasaka mashabiki waliofanya uharibifu wa miundombinu ikiwemo uvunjwaji wa viti katika Uwanja wa Taifa, uliofanyika Jumamosi iliyopita katika mechi ya Simba na Yanga.
Kamanda Sirro amesema kuwa, licha ya Waziri mwenye dhamana ya michezo, Nape Nnauye kutoa maagizo kwa timu husika kulipa gharama za uharibifu wa miundombinu ya uwanja huo, jeshi lake halitasita kuwatafuta waliohusika kwa kuwa wamefanya uvunjifu wa sheria.
Amesema Jeshi la Polisi lina mkanda wa video unaoonyesha watu waliohusika na uharibifu huo na kwamba polisi wako katika uchunguzi ili kuwakamata watuhumiwa hao na wakishapatikana watachukuliwa hatua za kisheria kwa kuwapeleka mahakamani.
Aidha, Kamanda Sirro amesema Jeshi la Polisi limebaini kuwa wahalifu wanatumia viwanja vya mpira kupanga mikakati ya kutekeleza uhalifu.
Amesema hivi karibuni polisi ilifanikiwa kukamata risasi 20 za silaha ya kijeshi aina ya G3 baada ya kubaini kundi la vijana waliokaa katika uwanja wa Mpira wa Azam uliopo Chamanzi kuwa ni wahalifu ambapo waliwafukuza pasipo kufanikiwa kuwakamata.
Amesema jitihada za kuwasaka wahalifu hao zinaendelea na uchunguzi wa risasi hizo unafanyika ili kubaini mahali zilikotoka
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment